WAZAZI WATOZWA FAINI KWA UTORO WATOTO SHULENI,WAO WATOA KILIO

0


 

Wakazi wa kata ya Mavanga iliyopo wiliya ya Ludewa mkoani Njombe wamewalalamikia walimu wakuu pamoja na Afisa elimu wa kata hiyo kwa kuwalazimisha kulipia fedha kwa mtoto atakayeshindwa kufika shuleni pamoja na kuwalipa walimu wa kujitolea.

Wakitoa malalamiko hayo mbele ya mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga alipofanya ziara katika kijiji cha Mavanga, Mbugani pamoja na kitongoji cha Luhuhu getini wananchi hao wamedai kuwa walimu hao wamekuwa wakiwatoza kiasi cha shilingi elfu tano kwa siku na endapo mwanafunzi hatofika shuleni siku tano basi wanatakiwa kulipa elfu 25,000.

Melania Mtweve ni mmoja wa wananchi hao ambaye ni mkazi wa kijiji cha Mavanga amesema wanashindwa kuelewa hizo fedha wanazitoa kwa malengo gani kwani wasipolipa watoto hurudishwa nyumbani mpaka aende na hiyo fedha.

" Kwa elimu ya mtindo huu ni bora watoto wangu wakaage nyumbani maana shule sasa hivi imekuwa ni mradi unaojitegemea ambao unawanufaisha walimu kwasababu mara nyingine mtoto anashinda shule kwa mambo ya msingi si kwa makusudi", Alisema Mtweve.

Read more>>>>>>>>>

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top