Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Peres Magiri ameagiza Halmashauri ya wilaya hiyo kununua risasi za kutosha ili kukabiliana na wimbi la Mbwa wanaoshambulia watu mitaani
DC Magiri ametoa agizo hilo katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya Kilolo leo tarehe 11,August 2021 ambapo amesema kuwa wimbi la mbwa kushambulia watu limeanza kuwa tishio wilayani humo
Takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwezi June mwaka huu watu 36 wamejeruhiwa kwa kushambuliwa na Mbwa zikiongezeka kutoka watu 24 Mwezi May.
Soma hii;GAZETI LA UHURU LAPOTOSHA, CCM WANG'AKA SABABU KUMZUIA RAIS KUGOMBEA 2025!