UKIKUTWA WAKALA WA UKAHABA KUKUMBANA NA KIFUNGO JELA.

0

Leo katika kona ya sheria Karibu tena tukufahmishe hili la UWAKALA WA UKAHABA na adhabu yake!.

KIFUNGU CHA 139 KANUNI YA ADHABU SURA YA 16.


Mtu yeyote ambaye- (a) analeta  au anajaribu kuleta mtu yeyote,  ikiwa ni mwanamke au mwanaume wa umri wowote,  kwa idhini au bila ya idhini yake  kuwa kahaba, ndani ya Jamhuri  ya Muungano au nje ya Jamhuri  ya Muungano;


Anamsababisha, au anajaribu  kusababisha mtu yeyote mwenye umri chini ya miaka kumi na  nane, kuondoka katika Jamhuri ya  Muungano, au bila ya ridhaa  ikiwa ni kwa au bila ya idhini ya  mtu huyo, au bila ya idhini kwa  nia ya kumsaidia ajihusishe na  ngono zisizo halali na mtu yeyote  nje ya Jamhuri ya Muungano, au  akimuondoa au kujaribu  kumuondoa kutoka katika  Jamhuri ya Muungano, mtu huyo,  kwa ridhaa yake au bila ridhaa  yake kwa nia hiyo;


Anasababisha, au kujaribu  kusababisha, mtu yeyote wa umri wowote, kuondoka katika  Jamhuri ya Muungano, kwa  ridhaa au bila ridhaa yake,  kwa  nia ya kwamba mtu huyo  atakuwa anaishi au anakwenda  kwenye danguro, mahali popote  au atamuondoa au kujaribu  kumuondoa mtu huyo kutoka  katika Jamhuri ya Muungano, kwa  ridhaa au bila ridhaa yake kwa  nia hiyo; anamleta, au anajaribu  kumleta katika Jamhuri ya  Muungano mtu yeyote mwenye  umri wa chini ya miaka kumi na  nane kwa nia ya kumshirikisha  kwenye ngono haramu na mtu yeyote hapa ndani au nje ya  Jamhuri ya Muungano;


Anasababisha, au anajaribu  kusababisha mtu yeyote wa umri wowote, kwa ridhaa au bila  ridhaa ya mtu huyo, kuondoka kwenye maskani yake anayoishi  katika Jamhuri ya Muungano ambayo si danguro, kwa nia ya  kumhusisha mtu huyo na ukahaba, kuishi au kuhudhuria  mara kwa mara kwenye danguro, ndani au nje ya Jamhuri ya  Muungano;


Anamfungia mtu yeyote bila  ridhaa ya mtu huyo kwenye danguro lolote au sehemu yoyote  kwa nia ya kufanya ngono haramu au udhalilishaji wa ngono kwa  mtu huyo, atakuwa ametenda  kosa la ukuwadi na akipatikana  na hatia atawajibika kwa adhabu  ya kifungo kisichopungua miaka  kumi na kisichozidi miaka ishirini au faini isiyopungua shilingi laki moja na isiyozidi shillingi laki tatu, au vyote  kwa pamoja.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top