BABA ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA KIFO CHA BINTI YAKE BAADA YA KUMLAZIMISHA KUOLEWA KWA FIMBO.

0

 

Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma linawashikilia Watu watatu akiwemo Baba mzazi Kulwa Juakali (40)  Mkazi wa kijijicha Lufubu Wilaya ya Uvinza kwa tuhuma  za kumpiga fimbo Mtoto wake Mbaru Juakali ( 17) hadi kusababisha kifo chake huku chanzo cha tukio hilo kikidaiwa kuwa ni kumlazimisha Mtoto huyo kuolewa chini ya umri  kwa mahari ya ng'ombe 13 bila ridhaa yake.

Kamanda wa jeshi la Polisi mkoani humo ACP James Manyama amesema tukio la mauaji lilitokea tarehe 10 novemba mwaka huu majira ya Saa mbili asubuhi katika kijiji hicho ambapo amesema binti Hugo aliuawawa baada ya kujeruhiwa kwa fimbo.

"Binti alipigwa sehemu mbalimbali za mwili wake akilazimishwa kuolewa ambapo kulikua na ahadi ya kulipwa mahari ya ng'ombe 13 na waliokua wakishinikiza aolewe ni wazazi na hao ndio walikua na uroho wa kupokea mahari ya hao ng'ombe 13, taarifa zilizopo binti huyu alikua anachumbiwa na Wanaume watatu kwa hiyo yule ambae ofa yae ilikuwa kubwa kwa ng'ombe 13 huyo ndio alikua analazimishwa aolewe nae wakati binti hakuridhia na kupelekea kipigo" amesema Manyama 


Polisi Mkoani Kigoma wanasema  upelelezi wa tukio hilo unaendelea na Watuhumiwa hao watafikishwa Mahakamani kwa hatua za kisheria akiwemo Baba mzazi Kulwa Juakali (40), Baba mkubwa wa marehemu Shija Juakali (44) na Baba mdogo wa marehemu aitwaye Majiba Juakali ( 29) wote wakazi wa kijiji cha Lufubu wilayani Uvinza mkoani Kigoma.



Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top