KUSHINDWA KUHUDHURIA KAMA SHAHIDI ADHABU SIKU "15" JELA.

0

SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA YA JINAI SURA YA 20 ILIYOREJEWA MWAKA 2019.

KIFUNGU CHA 147.

Mtu yeyote aliyeitwa kuhudhuria kama shahidi ambaye, bila sababu ya msingi, anashindwa kuhudhuria kama alivyotakiwa na wito au ambaye, baada ya kuhudhuria, anaondoka bila kupata ruhusa ya mahakama au anashindwa kuhudhuria baada ya kuahirishwa kwa mahakama baada ya kuamuriwa kuhudhuria, atawajibika kwa amri ya mahakama kulipa faini isiyozidi shilingi elfu tano.


 Faini iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha kwanza inaweza kutozwa kwa kushika na kuuza mali yoyote inayohamishika inayomilikiwa na shahidi ambayo iko ndani ya mipaka ya eneo la 

mamlaka ya mahakama.

 

Ikishindana kupata faini kwa kushika mali na kuuza shahidi anaweza, kwa amri ya mahakama, kufungwa kama mfungwa wa madai kwa kipindi cha siku kumi na tano isipokuwa kama faini imelipwa kabla ya kuisha kwa kipindi hicho.


Kwa sababu nzuri itakayoonyeshwa, Mahakama Kuu inaweza kusamehe au kupunguza faini yoyote iliyotolewa chini ya kifungu hiki na mahakama ya chini.


Imeandikwa na,

Mwanasheria

Johnson Yesaya Mgelwa @yesayajm_

Wa Jungu la sheria Tanzania

0758218269/0628729934.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top