Bila shaka wewe ni mhanga wa Ndugu kuhamia kwako,au hutamani Ndugu waweke kambi nyumbani kwako kwa sababu mbalimbali,Leo nakuletea mbinu kadhaa Zita lazily said is Ndugu wasikae muda mrefu kwako!
NB;Sikatai Ndugu kuja kukaa kwako ila kuna mipaka na wakati gani anaweza kuja kukaa kwako,hili ndilo la kuzingatia ila unawwza usikubaliane na hoja hizi ukatafuta zingine,tofauti na hizi karibu.
1. Hakikisha wageni ambao ni mke na mme hawalali chumba kimoja. ( Mimi kwangu dada yangu au mtu yeyote anayekuja kwangu na mkewe huwa nawapangia vyumba tofauti vya kulala, mwanaume analala chumba cha nje na mwanamke alale na house girl) kutokana na kero hii huwa hawachelewi kuaga.
2. Mgeni bachelor wa kiume hakikisha analala chumba cha ndani kabisa ili asipate muda wa kujinafasi kwenda kuangalia mipira (usithubutu kumpa chumba cha nje itakuwa furaha sana kwake atajisahau)
3.Kama huna vyumba vya kutosha wapeleke wakalale gest ( waulize wanakaa siku ngapi halafu lipia)
4. Usiwatambulishe wageni kwa mbwa wako, ( wabaki na hofu ya mbwa hadi watakapoondoka)
5. Mama mwenye nyumba usimpe zamu mgeni wa kike apike (asije akalizoea jiko akasahau kurudi kwao wacha asijisikie huru)
Je! Unakubaliana kwa asilimia ngapi kwa hoja hizi,kama unamaoni tuandikie kwenye bosi La. Comments hapo chini