UKITANGAZA ZAWADI ILI KUREJESHWA MALI ILIYOIBWA NI KOSA.

0

KIFUNGU CHA 113 CHA KANUNI YA ADHABU SURA YA 16 ILIYOREJEWA MWAKA 2019 KINASEMA;


Mtu yeyote ambaye-

(a) anatangaza kutoa zawadi kwa  kurejesha mali yoyote ambayo imeibiwa au imepotea, na katika kutoa zawadi hiyo ametumia maneno ikionyesha kwamba hakuna maswali yatakayoulizwa, au huyo mtu anayetoa mali hiyo hatakamatwa au kudhuriwa; au 

(b) anatangaza hadharani kumrejeshea mtu yeyote ambaye atanunua au ametanguliza  malipo ya fedha kwa njia ya kukopa kwa ajili ya mali yoyote  iliyoibwa au kupotea, mali hiyo  iliyolipwa au kutanguliwa au kiasi  kingine chochote cha fedha au zawadi kwa ajili ya kurejeshwa  kwa mali, au 

(c) anachapisha au anatangaza ahadi kama hiyo, kama ilivyotajwa katika aya ya (a)  au (b), atakuwa  ametenda  kosa.


Imeandikwa na Mwanasheria

Johnson Yesaya Mgelwa (@yesayajm_)

Wa Jungu la sheria Tanzania

0758218269/0628729934

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top