Jumuiya ya wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) mkoa wa Njombe inasikitishwa na vitendo vinavyofanywa na watu wasiojulikana kwa kubomoa ukuta wa ukumbi unaojengwa na Jumuiya hiyo wilaya ya Makete na kuwarudisha nyuma katika hatua za ujenzi huo.
Viongozi Wa UWT wakikagua ujenzi Wa jengo hill lilobomolewa ukuta wilayani Makete. |
Akizungumza na wajumbe wa baraza la wanawake wa wilaya hiyo mara baada ya kamati ya utekelezaji UWT kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo,Mwenyekiti wa Jumuiya Bi,Scolastika Kevela amesema kitendo kinachofanywa na watu hao hakikubaliki kwa kuwa kimekuwa kikirudisha nyuma jitihada za maendeleo ya ujenzi.
Akizungumza kwa niaba ya wanawake wa wilaya ya Makete mwenyekiti wa jumuiya wa wilaya hiyo Bi,Erika Sanga ameomba kusadiwa ili jingo hilo liweze kukamilika huku akitoa rai kwa wanamakete kuendelea kushirikiana ili kufanikisha ujenzi huo utakao kuwa na tija ndani ya wilaya.
Licha ya changamoto hiyo mkuu wa wilaya ya Makete Juma Sweda mara baada ya kutembelewa na kamati ya utekelezaji,amesema halmashauri ipo tayari kuendelea kuwasaidia wanawake katika kukuza uchumi ikiwemo kuwasaidia mikopo ili kuanzisha viwanda vidogo vidogo.
Kamati ya utekelezaji UWT mkoa wa Njombe imefika wilayani Makete na kukagua miradi ya jumuiya pamoja na kutoa elimu ya ujasiliamali juu ya ufugaji wa kuku kwa wanawake ili kufikia malengo yao ya kiuchumi.