WATUMISHI KUANZA KUKATWA FEDHA YA MSHAHARA KUCHANGIA MFUKO WA KUFA NA KUZIKANA

0

  Baraza la Wafanyakazi Manispaa ya Mtwara-Mikindani kwa pamoja limeridhia kuanzisha mfuko wa kufa na kuzikana kwa watumishi na kupendekeza kila mtumishi Kuchangia shilingi elfu mbili kila mwezi ambayo itakatwa kwenye mshahara wake
Akiwasilisha hoja hiyo kwenye Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika Novemba 10,2021 Katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Mtwara-Ufundi , Katibu wa Baraza la Wafanyakazi Manispaa ya Mtwara-Mikindani Justine Mkwara amesema kuwa mfuko huo unaanzishwa ili kuleta usawa kwenye masuala ya kupeana pole pindi mtumishi anapopatwa na msiba na kuondoa utaratibu unaotumika Sasa wa kupitisha karatasi ya Kuchangia rambirambi kwenye Ofisi.

Ameendelea kusema kuwa mfuko huo utatoa shilingi 500,000 pindi mtumishi atakapofariki au kufiwa na ndugu wa karibu wakiwemo baba, mama, mke,mume pamoja na Watoto wanne ambao mtumishi atakuwa amewaandikisha kwenye orodha ya wategemezi itakayoandaliwa na kwamba fedha zitakazokusanywa zitawekwa kwenye akaunti maalumu na kusimamiwa na kamati maalumu ya watu wasiozidi watano.

Kwa upande wake Afisa Utumishi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani Bi. Tamko Mohamedi  amesema kuwa uwepo wa mfuko huo haiondoi stahiki kama hizo anazostahili kuzipata mtumishi kutoka kwa mwajiri na kusisitiza kuwa mfuko huo ni wa hiyari hivyo wanufaika ni watumishi ambao wataridhia kukatwa kwenye mshahara kwa kujaza fomu maalumu.

Aidha amewataka Wajumbe wa Baraza hilo kila kmmoja kwa uwakilishi wake akafikishe hoja hiyo kwa watumishi anaowawakilisha ili kila mtumishi  aweze kuridhia kujiunga na mfuko huu muhimu wa kufa na kuzikana


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top