Jeshi la Polisi Mkoani Tanga linamshikilia Mohamed Lukindo (43) kwa tuhuma za kumuua Athuman Dolly baada ya kumfumania na Mke wake nyumbani kwake majira ya saa tusausiku wa kuamkia leo.
RPC wa Tanga Safia Jongo amethibitisha kutokea Kwa tukio hilo alfajiri ya kuamkia leo na kusema tukio hilo limefanyika katika Mtaa wa Vunja Bei Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga
"Mtuhumiwa alikuwa safarini zaidi ya mwezi mmoja na nusu na alirudi nyumbani kwake ghafla usiku wa kuamkia leo, aligonga nyumba yake lakini Mkewe alisita kufungua ndipo alipochukua uamuzi wa kuvunja mlango na kumkuta Mwanaume huy kwenye kitanda chake na kumpiga hadi kumuua" RPC Jongo
Je! Ulitazama video hii,kama bado bofya kutazama