Mtoto huyo anadaiwa kuzikwa na mama yake mzazi aitwaye Rebecca Siowi (30) usiku wa kuamkia Aprili 22, 2022 nyumbani kwa bibi yake walikokuwa wakiishi yeye pamoja na mama yake baada ya mume kumtelekeza na watoto watano.
Tukio hilo liligundulika baada ya mtoto huyo kutoonekana jioni ya Aprili 21 nyumbani alikokuwa akiishi kwa bibi yake, ambapo bibi yake huyo alifanya jitihada za kumtafuta mjukuu wake huyo bila mafanikio ndipo Aprili 22 alipobainika kuwa amezikwa.
Akizungumzia tukio hilo leo Aprili 23, 2022 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amekiri kuwepo kwa tukio hilo, akisema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo kutoka kwa wananchi walifika eneo la tukio kuona sehemu alipozikwa mtoto huyo.
Kamanda Maigwa amesema walipofika eneo la tukio walilazimika kuomba kibali cha kuufukua mwili wa mtoto huyo ili kujua sasababu hasa za kifo cha mtoto huyo kutokana na maneneo ambayo yalikuwa yakisemwa mtaani.
"Hili tukio kweli lipo na baada ya Jeshi la polisi kupata taarifa juu ya tukio hilo tulienda kuomba kibali cha kufukua mwili wa mtoto ili kujiridhisha sababu za kifo cha mtoto huyo ni nini kutokana na maneno mengi yaliyokuwepo mtaani.