MTOTO AMUUA BABA YAKE KWA KUMFUMANIA NA MKEWE CHUMBANI KWAKE!

0

JESHI la Polisi mkoani Shinyanga, linamshikilia kijana Mwandu Shija (32) mkazi wa Ndala Manispaa ya Shinyanga, kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi Shija Robert (55) kwa madai ya kumfumania akiwa amelala na mkewake kitandani.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga George Kyando, akitoa taarifa  kwa vyombo vya habari, alisema wakati kijana huyo aliporudi nyumbani ndipo akamfumania  baba yake akiwa amelala na mkewake na kuanza kumshambulia.

Alisema wakati kijana huyo akiendelea kumshambulia Baba yake na kipande cha kuni sehemu mbalimbali za mwili wake, ndipo alipompiga sehemu mbaya na kusababisha mauaji.

“Chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi, baada ya marehemu kukutwa akiwa amelala kitanda kimoja na mke wa mtuhumiwa,”alisema Kyando.

“Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na daktari na kuhifadhiwa katika Hospitali ya rufani mkoani Shinyanga, ukisubili kukabidhiwa kwa wanandugu kwa ajili ya mazishi,”aliongeza.

Aidha, alisema Jeshi la Polisi mkoani humo bado linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo, na utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

Na;Marco Maduhu.
 
TAZAMA VIDEO HII YA MBUNGE JIMBO LA MAKETE ISIKUPITE

 
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top