Diwani aliyepotea akutwa nyumbani kwa Ashura

0

 Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema polisi imefanikiwa kumpata diwani wa Kawe (CCM), Mutta Rwakatare aliyekuwa akitafutwa na ndugu zake kuanzia Februari mwaka huu.

PICHA KUTOKA MAKTABA

Hivi karibuni Meya wa Kinondoni, Songoro Mnyonge akiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani aliviomba vyombo vya dola, wanahabari kusaidia kumtafuta diwani huyo ambaye ni mtoto wa marehemu Dk Getrude Rwakatare.

“Tunamtafuta diwani wetu wa Kata ya Kawe hatujamuona muda mrefu, nyumbani hayupo, ofisini hayupo, kwenye chama hayupo, taarifa tunaambiwa amefichwa sasa sijui nani kamficha. Tunamtaka huyo aliyemficha diwani amuachie kwasababu anamnyima nafasi ya kuwatumikia wananchi amuachie na vyombo vya dola mtusaidie” alisema Mnyonge.

SOMA HII: SABABU ZA WANAWAKE KUBRID DAMU NYINGI NA MUDA MREFU.

Lakini leo Jumanne Mei 24, 2022 wakati akizungumza na wanahabari, Kamanda Muliro amesema baada ya uchunguzi wa polisi walifanikiwa kumpata Mutta (43) Mei 23 maeneo ya Tabata akiwa katika nyumba ya mwanamke mmoja aitwaye Ashura ambaye amedai ni rafiki yake wa siku nyingi.

Kamanda Muliro alisema, “alifika (Mutta) kwa Ashura Mei 19 mwaka huu akiwa katika hali ya ulevi uliopindukia.

“Kutokana na mazingira ambayo diwani huyo amekutwa nayo na maombi yaliyotolewa na ndugu kwa Jeshi la Polisi kwa ajili ya matibabu, pia walitoa kumbukumbu za nyuma za mwenendo na tabia za Mutta polisi limemkabidhi kwa ndugu zake kwa ajili ya matibabu na tiba za kisaikolojia,” amesema Muliro.

SOMA HII: SABABU ZA WANAWAKE KUBRID DAMU NYINGI NA MUDA MREFU.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top