Wanaume wengi hunyamaza wakati wanapoanza kuathiriwa na tatizo la kushindwa kutekeleza wajibu wao katika ndoa ikiwemo tatizo la kushindwa kushiriki tendo la ndoa.
Hivyobasi mara nyingi hulazimika kujiondolea lawama hiyo na badala yake kusema kwamba kizazi cha wake zao ndicho chenye tatizo.
Utafiti umeonesha kwamba wanaume wenye kati ya umri wa miaka 18 hadi 35 ni asilimia 15 ya idadi ya watu.
Vilevile wanaume wenye zaidi ya umri wa miaka 40 ni asilimia 40 ya wale wasioweza kuwatosheleza wake zao kindoa kutokana na tatizo linaloathiri sehemu zao za siri. (uume kushindwa).
Hali hiyo humfanya mwanaume kuhisi kukejeliwa na jamii ambayo hubeza hali hiyo.
Mwanaume au mwanamke aliye katika hali hiyo pia anaweza kukejeliwa au kupokea shutuma chungu nzima kutoka kwa jamii iwapo siri yake itajulikana nyumbani ama mahala popote pale.
Kutokana na hilo wanaume ambao hujipata katika hali hiyo ya kiafya hupendelea sana kutoshiriki katika mjadala kuhusu suala hilo kwasababu hujihisi kukatishwa tamaa.
Kunapotokea hali kama hiyo , magonjwa mengine pia huanza kumwathiri mwanaume kama huyo na mara nyingi huogopa kushiriki na wake zao katika tendo la ndoa.