Mtoto Mwingine Ashambuliwa na Kujeruhiwa Vibaya na fisi

0


Mtoto Gindu Kululu (06) Mkazi wa Bariadi

Matukio ya Fisi kushambulia watoto na kuwajeruhi vibaya maeneo ya usoni na kichwani yamezidi kushamili katika mji wa Bariadi, ambapo mapema asubuhi ya leo mtoto mwingine jina ni Gindu Kululu (06) mkazi wa mtaa wa Iyoma kata ya Somanda Halmashauri ya Mji wa Bariadi ameshambuliwa na myama huyo.

Fisi ameuawa kwa jumla ya risasi sita

Wazazi wa mtoto huyo wanaeleza kuwa majira ya Saa 8:00 kamili Asubuhi nyumbani mtoto huyo akiwa na mdogo wake nje, gafla alivamiwa na fisi huyo ambaye alitokea vichaka vilivyopo karibu na nyumbani.


Mganga Mfawidhi Hospitali ya Mji wa Bariadi Emmanuel Costantine amethibitisha kupokelewa kwa mtoto huyo na hali yake ilivyo.

Baada ya kutokea kwa tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Lupakisyo Kapange akiwa na kikosi cha Askari wa kutuliza gasia (FFU) walianza msako wa kumtafuta fisi huyo na kumpata hadi kumuua.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top