AMFUMANIA NDUGU YAKE AKIFANYA MAPENZI NA MKE WAKE NA KUMUUA

0
Kijana mmoja Aitwae Ibrahimu Nicodemas (22) Ameuawa na Binamu yake aitwae Thomasi Amsii (31) mtaa wa Sawe kata ya Maisaka wilaya ya Babati mkoani Manyara baada ya kumkuta binamu yake akifanya mapenzi na mke wake chumbani kwake.
PICHA KUTOKA MAKTABA

Akizungumza na kitruo cha redio @wasafifm mwenyekiti wa wa mtaa huo Michael John amekiri kutokea kwa tukio hilo kwenye mtaa wake nakusema kuwa baada ya kutokea kwa mauaji hayo alichukua jukumu la kuzungumza na mtuhumiwa sababu ya kuchukua jukumu la kumuuwa binamu yake nakusema alimkuta marehemu yupo na mke wake chumbani wanafanya mapenzi ndipo mtuhumiwa akachukua kisu na kumchoma upande wa kushoto wa kifua bila kukusudia

Pia tumefanikiwa kuzungumza na mama wa marehemu Agnesi Yona ambae amesema amekuja kujua kifo cha mtoto wake baada ya kuambiwa na mwenyekiti akiwa anaenda kwenye shughuli zake hivyo amelaani tukio hilo kwakuwa marehemu na mtuhumiwa ni mtu na ndugu yake

Kwa upande wao mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa tukio hilo lilitokea nyumbani kwa mtuhumiwa ambapo marehemu alikua na mke wa mtuhumiwa ndipo alipokutwa mara baada ya mtuhumiwa kurudi nyumbani kwenda kuchukua vifaa vya kazi yake

Licha ya mtuhumiwa kujisalimisha mwenyewe kituoni @wasafifm tunaendelea kufuatilia tukio hili kwa upande wa jeshi la polisi ili kujua kauli yao juu ya tukio hilo.

Chanzo;Wasafi fm

USIPITWE NA VIDEO ZETU KWENYE YOUTUBE YETU TAFADHALI BOFYA VIDEO HII
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top