DC MAKETE AMTAKA DMO AWARUDISHIE WANACHI GARI LA WAGONJWA

0

Mkuu wa Wilaya ya Makete Mh. Juma Sweda ameagiza gari la Kituo cha Afya Ikuwo lirudishwe Kituoni hapo mapema iwezekanavyo kwa lengo la kutoa huduma kwa wagonjwa.



Ametoa agizo hilo kwa Mganga Mkuu Wilaya ya Makete baada ya kufika Kata ya Ikuwo na kukutana na malalamiko ya wananchi wa Tarafa ya Ikuwo ambao wamesema wanapata changamoto kubwa ya usafiri wakati wanapopata dharura ya wagonjwa

Imeelezwa kuwa gari hiyo ipo kwenye Matengenezo Wiwlayani kwa muda sasa na inakaribia kukamilika

Wananchi wa Kata ya Ikuwo na Kigala wamekuwa wakitegemea gari hilo kupata huduma ya kusafirisha wagonjwa kwa gharama ndogo kwa kusafirisha wagonjwa kupeleka Hospitali ya Wilaya, ambapo kwa muda wa zaidi ya miaka mitatu wamekosa huduma hiyo

Baada ya wananchi wa Tarafa ya Ikuwo kuwasilisha changamoto ya Barabara ya Usalimwani, Ikuwo-Nkenja kwa Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhandishi kutoka TARURA Ndg. John Kawogo amesema serikali imetenga fedha Milioni 140 kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Usalimwani, Ikuwo mpaka Nkenja

Mhandisi Kawogo amesema tayari Ujenzi wa Barabara kutoka Usalimwani mpaka Ikuwo unaendelea na wanategemea kuanzia mwezi wa nane 2022 wanatarajia kuanza Matengenezo kutoka Matenga kuelekea Nkenja.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top