Amesema hayo wakati wa
makabidhiano ya pikipiki 69 zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza
majukumu yao leo tarehe 20 juni 2022 kwenye ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya
Makete.
Mh. Sweda amesema
maafisa ugani hao wanapaswa kutumia pikipiki hizo kwa kuzingatia maadili ya
utumishi na kuhakikisha lengo la Serikali linatimia kwa kuwahudumia wananchi.
“Niwasihi maafisa ugani wote matumizi ya pikipiki hizi yawe sahihi na tukibaini unafanya kazi ya kubeba abiria badala ya kwenda shambani kuwahudumia wakulima, hapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yako”
“Asilimia 70 ya watanzania
tunategemea kilimo ambacho ndio uti wa mgongo kwenye Taifa letu, Rais Samia
Suluhu Hassan ameona umuhimu wa kuwasaidia wakulima sasa tafadhali msimuangushe
kwenye jambo hili” ameongeza Mh. Sweda
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Makete Ndg. William Makufwe ameishukuru Serikali ya
awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kugawa pikipiki hizo kwa
maafisa ugani nchini.
“Pikipiki hizi
zinagawiwa kwa maafisa ugani 69 wote ndani ya wilaya yetu lakini hapo awali
tulikuwa na pikipiki 21 tu, napenda kumshukuru Rais kwa kuwajali maafisa ugani
ambao sasa wataweza kuwafikia wakulima tena mkulima mmoja mmoja ili kujua
changamoto zao, kuwapa ushauri na melekezo sahihi ya kilimo katika Wilaya yetu
na maeneo mengine”
Awali akisoma taarifa
fupi Afisa kilimo Wilaya ya Makete Ndg. Aniseti Ndunguru amesema Wizara ya
Kilimo imetoa pikipiki hizo ikiwa na lengo la kuwawezesha maafisa ugani ili
waweze kuwafikia wakulima na kutoa elimu ya kilimo bora.
“Tunatarajia tutapata
takwimu sahihi za uzalishaji, kilimo chenye tija na biashara huku tukitarajia
kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya Kilimo kwa asilimia 10 mpaka ifikapo
mwaka 2030 kwa uimarishaji unaofanywa na serikali upande wa Kilimo”
Afisa Ugani Kata ya
Itundu ndg. Steven Ngoloka kwa niaba ya maafisa Ugani Wilaya ya Makete
ameishukuru Serikali kwa kugawa pikipiki hizo ambazo amesema zinakwenda
kubadilisha kilimo kwa wanamakete kuanzia sasa.
“Pikipiki hizi
zitatufanya tufike kwa wakulima wengi zaidi, haraka na kuweza kuwasikiliza
wakulima wetu changamoto zinazowakabili na kuzitatua mapema, tunaishukuru
Serikali kwa kutambua umuhimu wetu kwa wakulima na tuihakikishie Serikali
kuleta mapinduzi makubwa kwenye Kilimo”