Ubakaji ni ZIMWI linaloendelea kuwatafuna wanafunzi wengi katika visiwa vya Zanzibar katika karne hii ya 21.
Kwa mujibu wa ofisi ya mtakwimu mkuu wa Serikali ya Zanzibar, matukio ya vitendo vya ubakaji ambayo yamekusanywa ikiwemo jeshi la Polisi, mahakama na vituo vya mkono kwa mkono jumla ya matukio 1,363 sawa na asilimia 34.45 wanafunzi wamebakwa mwaka 2020.
Kwa upande wa Mkoa wa Kusini Pemba pekee ambapo Makala hii ndipo inapoangazia vitendo vya ubakaji kwa watoto jumla ya matukio ya ubakaji kwa watoto 272 yameripotiwa kutoka mwezi January hadi Disemba mwezi 2022, sawa na asilimia 12.09.
Mwanafunzi wa darasa la Saba (7) mwenye umri wa miaka kumi na saba (17) jina limehifadhiwa ambaye March 27, 2022 aligunduliwa kuwa na ujauzito wa miezi Saba nusu huko Jombwe Mwambe Kisiwani Pemba, amejifungu Mtoto wa kike baada ya miezi tisa ya ujauzito kukamilika.
Picha kutoka Maktaba
Akizungumz na idawaonline.com Mama mzazi wa Mtoto huyo amesema Binti yake aliyekuwa akisoma darasa la Saba (7) ambaye inadaiwa alipewa ujauzito na Kijana aitwaje Makame Omar Bakari 30, tarehe 10 mwezi May amejifungua salama baada ya kuulea ujauzito huo kwa kipindi cha miezi tisa (9).
Amesema licha ya kuripoti Kituo cha Polisi Kengeja kuhusiana na tukio Hilo hakuna hatua yoyote ambayo ilichukuliwa Kwa ajili ya kumtia mtuhumiwa mbaroni.
"Tulitoa taarifa Kituo Cha Polisi Kengeja pamoja na Kituo Cha Polisi Madungu Chake Chake lakini Hadi hii Leo Mtoto wangu anajifungua" alisema Mama huyo
Aidha amesema hali ya mama mzazi pamoja na kichanga hicho zinaendelea vizuri hadi muda huu.
BABA MZAZI WA BINTI ALIYEJIFUNGUA
Nae Baba mzazi wa binti huyo amesema wamesikitishwa na kitedno cha binti yao kukatishwa masomo nakuomba mtuhumiwa kuchuliwa hatua kali za kisheria wakati atakapotiwa mbaroni.
‘’kwakweli suala hili limetusikitisha sana kwasababu mtoto wetu bado ni mdogo sana alitakiwa sasa hivi awe anaendelea na masomo lakini amekatishwa masomo pamoja na ndoto zake” ameleeza
JESHI LA POLISI MKOA WA KUSINI PEMBA
idawaonline.comilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Richard Tadeo Mchomvu ili kufahamu juhudi walizochukua ili kumtia mbaroni mtuhumiwa huyo lakini hakuweza kuweka wazi hatua wazochukua za kumtia mbaroni mtuhumiwa huyo.
MSAIDIZI WA HUDUMA ZA SHERIA WILAYA WILAYA YA MKOANI.
Bimkubwa Mohammed Ali ni msaidizi wa huduma za sheria Wilaya ya Mkoani na mwanaharakati wa wanawake na watoto, amesema kutokuchukuliwa hatua Kwa watuhumiwa wa Vitendo vya udhalilishaji ni Moja miongoni mwa sababu zinazopelekea vitendo hivyo kuongezeka
"Tunaposema vyombo vya Sheria ni pamoja na Jeshi la Polisi pamoja na madawati ya jinsia lakini mpaka sasa hivi wako kimya hakuna hatua ambayo wamechukua, kwahivyo ni kama limepuuzwa upande mmoja" aliongeza
MAJIRANI WA MSICHANA ALIEJIFUNGUA
Nao majirani wa Binti huyo wamesema kitendo Cha Binti huyo kupewa ujauzito kimewahuzunisha sana ukizingatia Bado Binti huyo ni mdogo na anaendelea na masomo.
"Kwakweli tumehuzunishwa Sana suala hili maana kwanza huyu mtoto bado ni mdogo sana na anasoma darasa la Saba, kwahivyo ameshamkatisha ndoto zake alizokuwa nazo Kwasababu hawezi kusoma huku ana ulezi wakati yeye mwenyewe bado ni mtoto labda anaweza kuendelea na masomo akishamuachiza" walisema majirani hao
MWALIMU MKUU WA SKULI YA MSINGI MWAMBE
Ali Mohammed Omar ni mwalimu wa Skuli ya msingi Mwambe ambayo alikuwa anasoma msichana huyo, amekiri kupokea taarifa za binti huyo kujifungua na kutoa taarifa hizo kwa afisa mdhamini wizara ya elimu na mafunzo ya amali Pemba.
Aidha amesema binti huyo alikuwa ni mwanafunzi mtulivu, mpole na mwenye kufuata taratibu zote za skuli na alikuwa na ufahamu wa wastani.
KAULI YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR
Mohammed Nassor Salim ni afisa mdhamini wizara ya elimu na mafunzo ya amali Pemba, amekiri kupokea taarifa za kujifungua kwa mwanafunzi huyo aidha amesema baada ya kumaliza siku arobaini (40) ya kujifungua anaweza kuendelea.
Licha ya fursa hiyo ya Wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar, kumtaka mwanafunzi huyo kuendelea na masomo baada kukamilika kwa siku 40 kutoka kujifungua lakini mwanafunzi huyo alishindwa kuitumia fursa hiyo ambayo ilionekana kuwa ni bahati ya dhahabu kupata haki yake ya msingi ya elimu pamoja na kutimiza ndoto zake.
“Ni kweli wizara alimpa fursa mtoto wetu wa kuendelea na masomo baada ya siku 40 kutoka kujifungua lakini kutokana na mazingira yetu hapa nyumbani na hali ya umasikini alishindwa kurudi skuli maana hawezi kwenda skuli wakati mtoto hana wa kumuachia maana mimi asubuhi mapema natoka nakwenda zangu shamba na baba yake anakwenda kutafuta ruzki sasa mtoto atamuachia nani” alisema mama wa mwanafunzi hyo
WATU WATANO WAFA KWA KUNYWA DAWA YA KUACHA KUNYWA POMBE..