ADEMASU AHUKUMIWA JELA NA WENZAKE 36 SIKU MOJA BAADA YA KUKAMATWA NJOMBE

0

 Na;Edwin Moshi Njombe 

Mahakama ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imewahukumu wahamiaji haramu 37 kifungo cha mwaka mmoja gerezani au kulipa faini ya shilingi laki 5 kila mmoja kwa kosa la kuwepo katika jamhuri ya muungano wa Tanzania bila pasport wala kibali

 

Washtakiwa hao Ademasu Mulatu (18) na wenzake 36 raia wa Ethiopia wameshtakiwa katika Mahakama hiyo baada ya kukutwa Julai 7,2022 katika kijiji cha Kidope wilayani Makete mkoani Njombe kinyume na kifungu cha 45 (1)(2) cha Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2016


Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo Mh. Ivan Msaki, mwendesha mashitaka wa polisi Benstard Mwoshe leo Julai 8, 2022 amewasomea washitakiwa wote shitaka lao ambapo wamekubali shitaka lao la kukutwa hapa nchini kinyume cha sheria

 

Wakijitetea kabla ya hukumu hiyo kutolewa washtakiwa hao wamesema walikuwa wakisafiri kuelekea nchini Malawi na sababu ya kuondoka nchini mwao ni kutokana na maisha magumu pamoja na ndugu zao kuuawa hivyo wanaiomba mahakama hiyo iwahurumie

 

Mh. Hakimu Msaki amesema mahakama hiyo imezingatia utetezi wao wa kuonewa huruma na mahakama hiyo hivyo akawahukumu Kifungo cha Mwaka mmoja jela ama kulipa faini ya shilingi laki 5 kila mmoja,na baada ya adhabu watatakiwa kurudi nchini mwao

 

Washtakiwa hao ni miongoni mwa wahamiaji haramu 69 waliokutwa Julai 7,2022 katika kijiji cha Kidope kata ya Iniho wilayani Makete mkoani Njombe baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali na kusababisha wahamiaji haramu wawili miongoni mwao kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa.

TAZAMA VIDEO HII ITAKULIZA WALEMAVU WANAVYOTENGWA KATIKA JAMII


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top