Mfanyabiashara Kijana wa Nakonde nchini Zambia mwenye umri wa miaka 29 ameanza kuandaa kaburi lake baada ya kuambiwa na Mganga wake wa Sumbawanga kuwa atakufa hivi karibuni kwa kukiuka masharti ya utajiri wake.
Grigory Siame ambaye alikuwa maskini sana hadi alipoenda kuonana na mganga miaka 8 iliyopita, anadaiwa kukiuka masharti baada ya kuabiri moja ya magari yake 5 mapya aliyonunua hivi karibuni na mganga kumpigia simu kuwa amekiuka masharti hivyo ajiandae kwa kifo..
Bw Siame tajiri kijana anamiliki saloon za kisasa za kiume 89 na vibanda vya simu za njiani BoothTelephone) 240 huko Nakonde na Tunduma ambapo hukusanya K28,000 sawa na TSH 3,975,000 kwa siku.
Pamoja na kumhisi sangoma (mganga wake) huyo amsamehe au kumbadilishia adhabu, Lakini juhudi zake hizo ziligonga mwamba,hivyo jamaa ameamua kuanza kuiandaa nyumba yake ya milele.
Kwa Sasa tajiri huyo mtoto anajiandaa kufa muda wowote hata ukimwangalia anaonekana Kuwa ni mtu aliyekata tamaa,tafadhali share kwa bofya link za social media iwafikie wengi.