JUKUMU LA MWANDISHI WA HABARI NI KUIBUA AJENDA ZENYE MASLAHI MAPANA KWA TAIFA- ALI MBAROUK.

Hassan Msellem
0

 Waandishi wa habari Kisiwani Pemba wamewatakiwa kuibua ajenda ambazo zitakuwa na maslahi kwa taifa ili kuwaongeza ushawishi katika Nyanja mbali mbali za maendeleo ikiwemo usawa wa kijinsia katika uongozi.

 

Akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya namna ya vyombo vya Habari na Utetezi katika ofisi za chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania ‘TAMWA’ Mkanjuni Chake Chake Pemba katibu wa klabu ya waandishi wa habari Pemba Ali Mbarouk Omar, alisema waandishi wengi wamekuwa na tabia ya kuripoti matukio mbali mbali yanayotokeza katika jamii, habari za mialiko ya kazi pamoja na ziara za viongozi na kuacha jukumu la kuibua ajenda mbali mbali zenye maslahi ya umma jambo ambalo husabisha wananchi kukosa haki zao.

 

Ameongeza kuwa kutokana na waandishi wa habari kuliacha jukumu la kuiba ajenda badala yake jukumu hilo limekuwa likitekelezwa na wanasiasa, viongozi wa Serikali pamoja wa watu maarufu, hivyo basi amewaomba waandishi hao kulifanyia kazi suala la kuibua ajenda zenye maslahi kwa umma ili kuongeza ushawishi katika mipango ya maendeleo.

 

“Jukumu la mwandishi wa habari ni kuhakikisha anaibua ajenda zenye maslahi mapana kwa umma kupitia vyanzo mbali mbali vya habari, lakini chakusikitisha ni kuona waandishi wengi wanakimbilia kwenye kuripoti matukio mbali mbali yanayojitokeza katika jamii, kuandika habari za mialiko pamoja na ziara za viongozi” alisema


Kwa upande wake, mratibu wa Tamwa Pemba Fathiya Mussa Said, alisema miongoni mwa sababu zinazopelekea wanawake wengi kushindwa kushiriki katika kugambania nafasi mbali mbali za uongozi ni pamoja na majukumu ya kifamilia na ukosefu wa huduma bora za kijamii ikiwemo ukosefu wa vitambulisho vya Uzanzibari mkaazi, Ukosefu wa maji safi na salama, huduma za afya na nishati ya umeme.

 

Akiorodhesha baadhi ya maeneo ambayo yanakabiliwa na changamoto za ukosefu wa huduma vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya Uzanzibari mkaazi ni pamoja Makaazi, Kiungoni, Konde, Wingwi, Tumbe, na Mtemani.

 Umesoma hii : How to Earn $500 daily from Google Translate

“Kwahivyo kuna changamoto nyingi sana zinazowakabili akina mama kushindwa kujiingiza katika vyama vya siasa pamoja kugombania nafasi mbali mbali za uongozi, ikiwemo ukosefu wa huduma bora za kijamii, Vyeti vya kuzaliwa, Vittambulisho vya Uzanzibari Mkaazi pamoja majukumu ya kifamilia, kwahivyo waandishi tunapaswa kuongeza nguvu ya utetezi katika vyombo vyetu ili kuona changamoto hizo zinafanyiwa kazi” Bi. Fathiya Mussa Said

 

Aidha alisema, watetezi wa jamii wa Wilaya ya Wete walifanikiwa kuibua changamoto ya ukosefu wa huduma ya kituo cha afya huko Mjini Kiuyu na kugundua uwepo wa jengo la kituo cha afya ambalo lilijengwa na wananchi na kuimba ofisi ya makamo wa kwanza wa pili wa rais Pemba kusaidia millioni 34,064500 kwa ajili ya umaliziaji wa jengo hilo.

 

Mratibu wa Tamwa Pemba Fathiya Mussa Said akiwasilisha mada ya changamoto zinazowakabili wanawake katika kombania nafasi mbali mbali za uongozi pamoja kutokujishughulisha na shughuli za kisiasa.


Wakichangia mada katika mafunzo hayo, baadhi ya waandishi wa habari wamesema ukosefu wa mazingira bora ya kufanyia kazi, hali za kiuchumi pamoja na kutokuwa wabunifu ni miongoni mwa sababu zinazochangia kutokufanya kazi zenye ubora na maslahi kwa umma.

 

“Ukiangalia unafanya kazi lakini huna usafiri wala ofisi unayofanya kazi hakuna usafiri kwa ajili ya waandishi, huna vifaa vyakufanyia kazi, huna nauli wengine ubunifu pia wakufanya hizo kazi hawana tunawezaje kuibua ajenda na kuifanyia utetezi” alisema mmoja wa waandishi hao

 

Mwandishi wa kituo cha Radio jamii Micheweni na Jamii Tv Ali Massoud Kombo akichangia mada katika mafunzo hayo.

Nao waandishi hao wameahidi kubadilika, kuyatoa mafunzo hayo kwa waandishi wenzao pamoja na kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili yaweze kuleta tija kwa taifa.


"kwakweli mafunzo ni mazuri sana yameongezea ujuzi wa kutosha, kwahivyo sasa waandishi ni jukumu letu kuyafikisha kwa waandishi wenzetu pamoja na kuyafanyia kazi napia tunaomba mafunzo haya yawe yanatolewa mara kwa mara ili tusiweze kuyasahau" Mchanga Haroub mwindishi wa ZBC.


Mwandishi wa Shirika la Utangazaji Zanzibar 'ZBC' TV Mchanga Haroub kwa niaba ya waandishi wenzake akiahidi kuyafanyia kazi mafunzo hayo.

 

KUHUSU MRADI

 

Mradi wa uhamasishaji wanawake kushiriki nasafi za uongozi ‘SWIL’ una lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake katika demokrasia ya uongozi katika ngazi za jamii na taifa kwa ujumla.

 

MALENGO YA MRADI

 

Ø Kuboresha uwezo wa wananchi 6000 ngazi ya jamii na taifa kuchukua hatua katika suala demokrasia na uongozi kwa wanawake.

Ø Kushirikiana na wasanii 400 katika uhamasishaji wa demokrasia kwa wanawake na haki ya kisiasa.

 Umeisoma hii : Get Paid $5.00 Per Video You Watch!! *FREE* (Make Money Online)

Ø Kuwawezesha waandishi wa habari 60 Unguja na Pemba kutoka vyombo tofauti kuandika habari za uchambuzi juu ya hali ya demokrasia na wanawake na uongozi.

 

Ø Kuwezesha mfumo wa usimamizi na tathmini katika kuwawezesha wanawake na uongozi pamoja na haki kisiasa.

 

WATEKEZAJI WA MRADI

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Tamwa, Zanzibar, Jumuiya ya Mazingira na Utetezi wa Kijinsia Pemba ‘PEGAO’ pamoja na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’.

WANUFAIKA WA MRADI

Wanawake, waandishi wa habari, jumuiya za kiraia pamoja pamoja na jumuiya ndogo ndogo zinazopatikana katika jamii.

WAFADHILI WA MRADI

Ubalozi wa Norway Tanzania.

MUDA WA MRADI

Miaka minne (4) kuanzia 2020 hadi 2023.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top