MBUNGE MWINYI ATOA ZAWADI KWA WANAFUNZI 35 WA JIMBO LA CHAMBANI WALIOFAULU KIDATO CHA NNE 2022.

Hassan Msellem
0

Wanafunzi 35 wa waliofaulu kidato cha nne mwaka 2022 katoka skuli tano za jimbo la Chambani wametakiwa kuongeza bidii katika masomo yao ili kuendelea kufanya vizuri katika mitahani ya kidato cha sita.

Akitoa zawadi ya mikoba, madaftari pamoja na sare kwa wanafunzi hao Mbunge wa jimbo wa la Chambani Mhe. Mohammed Abrahmani Mwinyi, amesema uongozi wa jimbo hilo umejitolea kwa dhati kuisaidia sekta ya elimu ili kuhakikisha wanafunzi wa jimbo hilo wanafanya vizuri katika masomo yao.

 

Aidha amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwakushirikiana na Serikali ya jamhuri ya Tanzania zimetoa fursa ya elimu bure kuanzia elimu ya darasa la saba hadi kidato cha sita ili kuhakikisha kila raia anapata haki ya msingi ya elimu.


“Munatoka hapa munakwenda hatua nyengine nawaomba acheni utoto 2024 tuhakikishe hakuna mwanafunzi aliyepata division zero kama mwaka huu tumepeta division one 6, 2024 tuhakikishe tunapata division One zote” Mohammed Abrahman Mwinyi

 

Kwa upande wake katibu mwenezi wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mkaoni Talib Bailal Shamte, amesema kutolewa kwa zawadi hizo ni kuwaongezea ari wananfunzi hao ili kuhakikisha wanafanya vizuri katika masomo pamoja na mitihani yao ya kidato cha sita.

 

“Tumeamua kuwapatia hizi zawadi ili ziwe ni chachu ya nyinyi kuwa na shauku na ari ya kuendelea kusoma kwa bidii ili muendelee kufanya vizuri katika masomo yenu na mitihani yenu ya kidato cha sita kwahivyo nawaombeni musome kwa bidii sana na sisi tuko nyuma yenu” Talib Bilal

 

Nae katibu wa CCM jimbo la Chambani Amour Kheri Vuai, amewataka wanafunzi hao kutokujiingiza katika suala la mapenzi ili kuimarisha msingi wa maisha yao ya baadae.

 

“Nawasihi sana kutokujiingiza katika suala la mapenzi kwasababu mukishajiingiza tu kwenye mapenzi safari ya masomo imeishia hapo kwahivyo sasa hivi kazi yenu iwe ni kusoma tu na sio vyenginevyo” Amour Kheri Vuai

Wanafunzi waliofaulu kidato cha nne 2022 Jimbo la Chambani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini.


Shaibu Ali Juma ni mwenyekiti wa CCM jimbo la Chambani , amesema kutolewa kwa zawadi hizo ni muendelezo wa kutekeleza kwa ahadi mbali mbali zilizotolewa na viongozi wa jimbo katika kuunga mkono juhudi za maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo.


Diwani wa wadi ya Ngwachani Mohammed Said Ali, amewaomba wanafunzi hao kuchagua masomo ambayo yataendana na fani ambazo wanajiandaa kusomea ili kwenda sambamba na fani hizo.

 

“Suala la kutambua ni nataka kuwa nani katika maisha yako ya baadae kisha ukatambua masomo ya kusoma ni muhimu sana kwani utakaposhindwa  kutambu unahitaji kuwa nani hapo baadae utashindwa kujua ni masomo gani muhimu ya kusoma” Diwani Mohammed Said

 

Nao wanafunzi hao wameushukuru uongozi wa jimbo hilo kwakuwapatia zawadi hizo na kuahidi kusoma kwa bidii ili kufanya vizuri katika mitahani yao ya kidato cha sita.

 

“Kwakweli tumefarijika sana kwakuaptiwa zawadi hizi na inatia moyo kuwa viongozi wa jimbo letu wako pamoja nasi kwahivyo tunaahidi kusoma kwa bidii ili kufanya vizuri katika mitahani yetu ya kidato cha sita” Aziza Amour Salehe kutoka Skuli ya Sekondari Ukutini

Mbunge wa Jimbo la Chambani Mheshimiwa Mohammed Abrahman Mwinyi akizungumza na wanafunzi waliofaulu kidato cha nne 2022.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top