RC MATAR; AAHIDI KUWASWEKA NDANI WAZAZI WANAOWATOROSHA WATOTO WAO AMBAO NI WATUHUMIWA WA MAKOSA YA UDHALILISHAJI.

Hassan Msellem
0

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Matar Zahor Massoud, amesema atawachukulia hatua kali za kisheria wanafamilia ambao huwatorosha ndugu zao ambao ni watuhumiwa wa makosa ya udhalilishaji ili kuhakikisha watuhumiwa wa makosa hayo wanadhibitiwa.

 

Ametoa kauli hiyo katika dua ya kuiyombea nchi juu ya kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji huko Gombani Chake Chake Pemba, amesema katika kipindi hiki kumeibuka tabia ya baadhi ya wanafamilia kuwatorosha ndugu zao ambao ni watuhumiwa wa vitendo vya udhalilishaji jambo ambalo linarudisha nyuma juhudi za kupambana na janga hilo.

 



“Kijana yeyote alitakayefanya vitendo vya udhalilishaji kisha akakimbia naomba munivumilie wakiwa ni wazazi wake au ndugu zake walioshiriki kumtorosha wote nawatia ndani” RC MATAR

 

Aidha amesema utafiti unaonesha kuwa watuhumiwa wa kesi za udhalilishaji ambao hutoroka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyengine huendeleza kufanya vitendo hivyo bila ya kujali alikotoka kufanya kosa hilo.

 

“Na utafiti wetu unaonesha hawa wanaofanya vitendo hivi vya udhalilishaji kisha kukimbia na huko wanakokwenda huendeleza kufanya vitenda hivyo kwa mfano mtuhumiwa akitoroka Pemba kwenda Unguja akifika Unguja anaendelea kufanya vitendo hivyo” alisema

 

 Kwa upande wake, Mratibu kutoka Ofisi ya Mufti Mkuu Pemba Sheikh Said Ahmad Mohammed, amesema miongoni mwa sababu zinazopelekea kukithiri kwa maasi mbali mbali katika jamii ni waislamu kuacha mwenendo wa kiongozi wa dini ya Kiislamu Mtume Mohammad s.a.w, hivyo basi amewaomba waumini wa dini ya kiislamu kufuata mwenendo wa kiongozi huyo ili kuepukana na maasi hayo.

 

Maasi na majanga yote haya yanayotukumba ni kwasababu tumeachana na mwenendo wa kiongozi wetu katika imani Mtume Muhammad sallawahu allayhi wasallam” Sheikh Said Ahmad


Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika Sala maalum ya kuliyombea dhidi ya kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji.

Nae Mwenyekiti wa Istiqama For Development Pemba Mohammed Suleiman Khalfan, amewaomba wazazi na walezi kufuata maelekezo ya dini ya kiislamu katika malezi ili kuwa na jamii yenye mustakbali mwema.

 

Mwenyekiti wa Bodi kutoka jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba (TUJIPE) Sheikh Abdalla Nassor Abdalla, amesema kumekuwa na tabia mbaya kwa baadhi ya akina mama ambao husimama barabarani kuomba msaada wa usafiri lakini baada ya kupatiwa msaada huo huwasingizia madereva kuwa wamefanyiwa vitendo vya udhalilishaji ili kujipatia fedha.

 

“Mheshmiwa mgeni rasmi sasa hivi nasikia kumezuka mchezo mchafu sana kuna akina mama ambao hukaa barabrani wakajifanya wanahitaji huduma ya usafiri ukimpa lifti waanza kupiga makelele kwamba wamebakwa tumefikia pabaya sana” alisema

 

Kutoka mwezi June 2021 hadi June 2022 takriban kesi 130 za udhalilishaji zimeripotiwa katika vituo mbali mbali vya Polisi katika Mkoa wa Kusini Pemba.

 

Dua hiyo ya kuiyombea nchi dhiya ya maasi na majanga mbali mbali imeandaliwa na jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba (TUJIPE) pamoja na Ofisi ya Mufti Zanzibar na KUhudhuriwa na viongozi wa Serikari, dini pamoja na wananchi mbali mbali.


Akina mama wa dini ya kiislamu wakiwa katika viwanja vya Gombani Pemba katika dua maalum ya kuiyombea nchi dhidi ya kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top