TAMWA KINARA WA KUPINGA SHERIA KANDAMIZI KWA VYOMBO VYA HABARI ZANZIBAR.

Hassan Msellem
0

Habari ni taarifa halisi juu ya matukio mbali mbali yanayojiri ulimwenguni ambayo mtu anahaitaji kusikia, kuona au kusoma kwa lengo la kupata taarifa Fulani.

 

Haki ya kutafuta, kutoa na kupokea habari ni haki ya msingi ya mwanadamu iliyoainishwa kwenye Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 18 (1) na (2) ambavyo vimeeleza kuwa kila mtu ana haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu matukio mbali mbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.


                                                 Picha kutoka Maktba


Vyombo mbali mbali vya Kimataifa vinatambua umuhimu wa haki ya kupata taarifa ikiwa ni pamoja na haja ya kuwa na Sheria madhubuti kwa ajili kulinda utoaji wa haki hiyo.

 

Vyombo hivyo ni pamoja na Umoja wa Mataifa (UN), Muungano wan chi za Amerika (OAS), Baraza la Ulaya (CE) na Umoja wa Afrika (AU).

 

Licha ya sheria, sera pamoja na mikataba mbali mbali juu ya uhuru na haki ya kutafuta taarifa na kuzisambaza kwa umma, lakini bado kuna sheria ambazo ni kandamizi kwa vyombo vya habari na wanahabari kwa ujumla.

 

Miongoni mwa Sheria hizo ni sheria nambari 5 ya 1988 ya Usajili wa Mawakala wa Habari, Magazeti na vitabu iliyofanyiwa marekebisho na sheria nambari 8 ya 1997, kifungu cha Sheria cha 27 (1) kifungu hichi kinampa mamlaka afisa yeyote wa Polisi kuweza kukamata gazeti lolote, popote litakapoonekana, lilipochapwa au kuchapishwa au ambalo kwa maoni yake atalituhumu kwamba limechapwa au kuchapishwa, kinyume na sheria hii.

 

 Kifungu hichi kinaonesha wazi jinsi ambavyo vyombo vya habari na uhuru wa wanahabari unavyoingiliwa na kukandamizwa kwakumpa mamlaka kupitiliza afisa yeyote wa Polisi ambaye kwa bahati mbaya anaweza kuwa hana taaluma ya habari wala utambuzi wa sheria zilizompa uhuru mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake au kulipiza kisasi.

 

WADAU WA HABARI WANASEMAJE JUU YA KIFUNGU HIKI.

 

Kwa upande wake mwandishi wa habari mwandamizi Zanzibar Rashid Omar Kombo, amesema kifungu cha sheria kinachomruhusu afisa wa Polisi kuchunguza mchakato wowote au utendaji wa masuala ya habari kinyume na hati ya mahakama ni Sheria zinazokinzanza na mikataba mbali mbali ya kikanda na kimataifa juu ya uhuru wa vyombo vya habari.

 

Kimsingi mataifa yote ya kidekrasia ambayo yanafuata misingi ya demokrasia na utawala bora masuala ya afisa wa polisi kukamata na kukagua yanahitaji idhini na vibali vya mahakama afisa wa Polisi hawezi kuwa yeye ndiye anatuhumu na yeye ndiye anakamata hiyo itakuwa ni Sheria ya ajabu” amesema

 

Fathiya Mussa Said ni mratibu wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Kisiwani Pemba (TAMWA), amesema uwepo wa kifungu cha sheria kinachompa mamlaka afisa yoyote wa Polisi kufanya ukaguzi wa majengo pamoja na kukamata gazeti ni kifungu cha sheria ambacho inakandamiza uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari kwa ujumla.

                                  Fathiya Mussa Said Mratibu wa Tamwa Pemba.


 Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mafunzo ya Habari SUZA Bi. Imane Duwe, amesema kifungu cha sheria kinachompa mamlaka afisa yoyote wa Polisi kukagua majengo na kukamata gazeti ni sheria iliyopitwa na wakati kulingana na mabadiliko ya teknolojia ya habari, hivyo basi amevitaka vyombo vya sheria kuifanyia marekebisho sheria hiyo.

 

“Kiufupi naweza kusema kwamba ni sheria ambayo inapaswa kufanyia marekebisho kwani imeshapitwa na wakati kulingana na uhataji uliyopo sasa hivi kutokana na aina ya vyombo tulivyonavyo” amesema


                        MAONI YA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI.

 

Bakari Mussa Juma ni mkuu wa gazeti la Zanzibar leo Kisiwani Pemba, ametoa ushauri kwa waandishi wa habari kuendelea kupaza sauti ili kufanyiwa marekebisho kwa sheria ambazo zinaonaka kukinzana na uhuru wa vyoombo vya habari na wanahabari.

 

“Hajalisha kwamba tumepiga kelele sana juu ya sheria hizi lakini tusichokee niwasihi waandishi wenzangu tuendelee kupaza sauti mpaka tuhakikishe kuwa zimefanyiwa marekebisho” Bakar Mussa

 

Mhariri wa Hits fm Radio   Moza Saleh Ali, ameeleza kuwa kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia sheria kama hizo ni sheria kandamizi kwa tasnia ya habari, hivyo basi ameviomba vyombo vya sheria kuzifanyia marekebisho sheria hizo.

 

“Kwa mujibu wa wakati tuliona nao sheria kama hizi zionanekana ni sheria kandamizi kwa vyombo vya kwasababu nyakati zimebadilika kwa wakati ule pengine inafaa ila kwa wakatii sheria hiyo haiyendani na mazingira” alieleza

 

KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI ZINA MAONI GAZI JUU YA KIFUNGU HIKI.

 

Ali Mbarouk Omar ni Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Pemba (PPC), amesema mkataba wa Afrika wa haki za binadamu na watu ya mwaka 1981 ibara ya 9 na 19 zinatoa haki ya mtu kutafuta na kupokea taarifa pasi na uhuru wake kuingiliwa, hivyo kuendelea kuwepo kwa wa sheria hiyo kuna kwenda kinyume na makubaliano ya mkataba huo, hivyo basi ameshauri sheria hiyo kufanyiwa marekebisho haraka iwezekanavyo.

 

Nae Katibu wa jumuiya ya waandishi wa habari za maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) Salma Said, amesema kuendelea kutumika kwa sheria zisizozingatia uhuru wa vyombo vya habari ni miongoni mwa sababu zinazopelekea waandishi wa habari kufanyiwa matendo mbali mbali ya unyanyasaji ikiwemo kutekwa, kupigwa na hata kuawa.

 

“Ukiacha na hicho kifungu cha 27 kuna sheria nyingi sana ambazo hazikuzingatia uhuru wa vyombo vya habari wala usalama wa waandishi wa habari na ndio maana waandishi wa habari leo wanatekwa kiholela, wanapikwa na wengine kuuawa” Salma Said

 

MAONI YA BARAZA LA HABARI TANZANIA-ZANZIBAR.

 

Shifaa Said Hassan ni afisa mdhamini Baraza la Habari Tanzania-Zanzibar (MCT) amesema katika utaratibu wa kisheria afisa wa Polisi anapaswa kupewa kibali na mahakama kukagua jengo au kukamata gazeti, hivyo basi Sheria ambayo inampa mamlaka afisa yeyote wa Polisi kukagua jengo na kukamata gazeti kwa kwa maoni yake ni sheria inayokwenda kinyume  uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari kwa ujumla.


“Katiba ya Zanzibar ya 1984 ibara ya 18 imeruhusu kila mwananchi kuwa huru katika kutafuta na kusambaza habari ndani na nje ya nchi wakati wowote bila ya kuingiliwa na mtu yeyote, sasa Sheria ya namna hiyo ni Sheria inayo kwenda kinyume na hata katiba yetu” alifafanua


         MAONI YA WAANDISHI WA VYOMBO MBALI MBALI VYA HABARI.

 

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari wamesema kuendelea kuwepo kwa Sheria zisizo rafiki kwa vyombo vya habari kutapelekea waandishi kufanyakazi kwa khofu, jambo ambalo litapelekea taarifa wanazoandika kukosa usahihi


“Kama afisa yeyote wa Polisi amepewa mamlaka ya kukagua na kukamata hadi daftari la kumbukumbu la mwandishi kuangalia ameandika kitu gani ni lazima waandishi tutakuwa na khofu na hatutofanya kazi kwa ufanisi” alisema mmoja wa waandishi hao

 

                Zuhura Juma Said mwandishi wa gazeti la Zanzibar Leo Pemba

 

MAONI YA WAUZAJI WA MAGAZETI KISIWANI PEMBA.

 

Baadhi ya wauza magazeti maarufu kisiwani Pemba, wamesema sheria inayomtaka mchapishaji wa magazeti yanayochapwa Zanzibar kuwasilisha nakala mbili kwa kwa mrajis kwa gharama zake kila siku anapochajisha gazeti ni Sheria inayorudisha nyuma biashara ya uuzaji wa magazeti pamoja kampuni za uchapaji.

 

“Aina hiyo ya Sheria inarudisha nyuma kwa kiasi kikubwa biashara ya uchapishaji wa magazeti pamoja na uuzaji, kwasababu na mchapishaji wa magazeti anatumia gharama na muda kuposti nakala hizo kila siku” muuza magazeti maarufu eneo la Chake Chake

 

MAONI YA WASOMAJI WA MAGAZETI.

 

Idawaonline.com ilizungumza na baadhi ya wasomaji wa magazeti kisiwani Pemba, juu ya sheria hiyo na kusema endapo Sheria hizo hazitofanyiwa marekebisho zitapelekea wananchi wengi kukosa habari kwa wakati, hivyo basi wamependekeza Sheria hizo kufanyia mabadiliko

 

‘’Kiasi kikubwa sana wananchi tunategemea vyombo mbali mbali vya habari kwa ajili ya kupata taarifa mbali mbali zinazojiri ndani na nje ya nchi punde tu zinapojiri sasa kama kuna Sheria kama hizo ambazo zinaonekana kuminya uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari kufanya kazi zao wananchi tutashindwa kupata habari kwa wakati” alisema mmoja wa wasomaji hao

 

NINI KIFANYIKE ILI KUREKEBISHA SHERIA HIZO.

 

Wadau wa habari nchini wamekuwa wakichukua hatua kadhaa ikiwemo kuandaa makongamano mbali mbali kushinikiza kufanyiwa marekebisho kwa sheria hizo hususan katika kuadhimisha siku ya uhuru wa habari duniani.

 

Miongoni mwa wadau hao ni pamoja na Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania (TAMWA-Zanzibar) na shirika la habari la Internews Tanzania kwakuazisha mradi wa miezi sita (6) kwakushirikiana na Waandishi wa habari Visiwani Zanzibar katika kuongeza uchechemuzi ili kufanyiwa marekebisho kwa sheria ambazo zinazonekana sio rafiki kwa vyombpo vya habari na wanahabari kwa ujumla.


Mwisho.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top