TAMWA YAWANOA UPYA WAANDISHI HABARI ZANZIBAR JUU KUANDIKA HABARI ZA UCHAMBUZI MRADI WA SWIL.

Hassan Msellem
0

Waandishi wa habari sitini (60) visiwani Zanzibar wameombwa kuboresha kazi wanazozifanya juu ya mradi wa uhamasishaji wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi (SWILL) ili kazi hizo ziweze kuleta mabadiliko chanya kwa jamii.

 

Mapema akifungua mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo wa kuandika habari za uchambuzi juu ya ushiriki wa wanawake katika nafasi mbali mbali za uongozi waandishi wa habari sitini (60) wa Zanzibar, Mkurugenzi mtendaji wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Dr. Mzuri Issa, amesema licha ya mafunzo pamoja na semina mbali mbali wanazozifanya bado jamii inakabiliwa na dhana potofu juu ya nadharia ya wanawake na uongozi, hivyo basi amewaomba waandishi hao kuboresha zaidi kazi zao ili ziweze kufikia malengo ya mradi huo.


Aidha amesema wingi wa majukumu ya kifamilia ni miongoni mwa sababu zinazopelekea wanawake wengi kushindwa kugombea nafasi za uongozi kwani hutumia muda mwingi katika utekelezaji wa majukumu hayo.

 

“Kuna sababu nyingi sana zinazopelekea wanawake wengi kutokufanikiwa kugombea nafasi mbali mbali za uongozi lakini miongoni mwa sababu hizo ni imani potofu kwa baadhi ya wanajamii juu ya mwanamke kujiingiza katika siasa pamoja na wingi wa majukumu ya kifamilia” Dr. Mzuri

 

Kwa upande wake mratibu wa Tamwa Pemba Bi. Fathiya Mussa Said, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwapiga msasa waandishi wa habari kuweza kuandika habari za uchambuzi ambazo zitaweza kuishawishi jamii pamoja na mamlaka mbali mbali kuweza kubadili muelekeo na mitazamo kuhusu wanawake na ushiriki wake katika siasa na upatikanaji wa demokrasia kataika uongozi.

 

“Kwahivyo waandishi watakapo pata mafunzo haya  wataweza kutumia vyombo vyao katika kuandika habari mbali mbali za uchambuzi, habari ambazo zitakuwa zina impact na data mbali mbali zinazoonesha  mafanikio na changamoto  za wanawake katika kugombania nafasi za uongozi” Bi. Fathiya

 

Akiwasilisha mada ya JINSIA na UONGOZI mwandishi wa habari kutoka gazeti la Zanzibar Leo na Blogi ya Pembatoday Haji Nassor Mohammed, amewasisitiza waandishi hao kuzidisha jitihada na ubinifu katika kuandika habari ambazo zitaweza kubadili mitazamo hasi kwa wanajamii ili kuhakikisha usawa wa kijinsia katika uongozi unapatikana

 

“Kwa mfano tumeona hapa katika sifa zote saba hakuna sifa ambayo imemtaja mwanamme hii ina maana kuwa suala la uongozi ni haki ya wanaume na wanawake, kwahivyo tunapoandika habari zetu tunapaswa kutoa elimu hii kwa jamii” Alisisitiza


Mwandishi wa Gazeti la Zanzibar Leo, Pemba Haji Nassor Mohammed akiwasilisha Mada kuhusu Jinsia na Uongozi.                                                                                               

Akitoa maelekezo juu ya namna ya kutengeneza vipindi bora vya radio na televisheni afisa habari na mawasiliano Tamwa Pemba Gaspery Charles, amesema mafunzo hayo ya siku tatu ni kutokana na mapungufu yaliyojitokeza katika kazi mbali mbali za waandishi wa habari juu ya mradi huo wa SWILL ikiwemo kukosekana kwa ubora wa sauti kwenye vipindi, ufuatiliaji mdogo, kukosekana kwa takwimu, uchache wa vyanzo vya habari, kukosekana kwa usawa wa kijinsia pamoja na uongezaji wa taarifa zisizo sahihi katika vipindi.

 

Amewaomba waandishi wa vyombo hivyo kuandaa muongozo mzuri wa vipindi wanavyoandaa ikiwemo kuwa na elimu ya wanawake na uongozi pamoja kufanya tafiti ili kuandaa vipindi na makala zenye maudhui bora.

 

Akichangia mada mwandishi kutoka shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) Mchanga Haroub, amesema moja miongoni mwa changamoto zinazowakabili waandishi habari juu ya uandaaji wa vipindi hivyo ni ukosefu wa vitendea kazi vya uhakika pamoja na mazingira yasiyo rafiki kikazi.

 

“Kwa mfano unamkuta mwandishi ana idea mzuri yakufanya lakini akiangalia hana vitendea kazi kwa mfano camera yenmye uwezo mzuri, usafiri au nauli kwa ajili ya kutafuta sources, sasa kwakweli katika mazingira kama hayo ni vigumu kupata makala bora” Mchanga Haroub

 

Nae mwandishi kutoka blogi ya Full Shangwe Masanja MAbula, amesema kutokufahamu lengo la uandaaji wa vipindi hivyo, kutokujituma pamoja na kutokuwa na ubunifu kwa waandishi wengi wa habari kuna changia kwa kiasi kikubwa kuandaa vipindi ambavyo havina ubora.

 

Nao waandishi hao wameahidi kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili kuzalisha vipindi ambavyo vitakuwa na ubora vitakavyoleta mabadiliko chanya katika jamii.

 

Mafunzo hayo ya siku 3 juu ya mradi wa uhamasishaji wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi (SWILL) yanajumisha waandishi sitini (60) ambapo ishirini (20) kutoka Pemba na arobaini (40) kutoka Unguja na kuandaliwa na chama cha waandishi wa habari wanawake Tamwa Znz, jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba (PEGAO) jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar (ZAFELA) kwa ufadhili wa UbALOZI WA Norway Tanzania.

 

Mafunzo hayo ya siku 3 yameanza rasmi July 20, 2022 na kutarajiwa kukamilika July 23, 2022.

Mratibu wa Tamwa-Pemba Fathiya Mussa Said akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya mafunzo ya siku 3 ya mradi wa SWIL.

Wasiliana nami Kwa simu Na. +255672270730\+255773360870.

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top