Mwanaume mmoja huko Afrika Kusini amejipatia umaarufu katika mitandao ya kijamii, baada ya kukimbia umbali wa Kilometa 90 kumthibitishia mpenzi wake Prudence kuwa amefika mwisho wa kutafuta na kwamba anataka wawe mume na mke.
Joseph Kagiso Ndlovu mzee wa miaka 57, amesema amekimbia umbali huo, ili ampose mwanamke aliyetajwa kwa jina la Prudence.
Joseph alipigwa picha akiwa ameshika bango la kumtaka mwanamke huyo amuoe, alipokuwa akikaribia kumaliza mbio za Comrades Marathon siku ya Jumapili.
“Prudence utanioa? Nimekimbia 90 kilometa kwa ajili yako,” aliandika katika bango.
*Mtandaoni kuna #fursa nyingi sana*Je umewahi kujiuliza lile #bundle lako ambalo unijiunga kila siku au wiki na hata mwezi limekunufaisha vipi? Au ndo vile unaingia mtandaoni kusapoti ndoto na maono ya wengine🌝? Basi badili mtazamo wako Leo anza kutimiza ndoto zako LeoJisajili na fursa <<hapa>>>>
Vyombo vya habari vya ndani na watumiaji wa mtandaoni wamekuwa wakihoji umbali, ambao mwanaume anapaswa kwenda kumtongoza mpenzi wake