DEREVA WA DALADALA MBARONI TUHUMA ZA KUUA KONDAKTA 'MPENZI WAKE'

0

 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Maarifa Matala mwenye umri wa miaka 45, ambaye ni dereva wa daladala na mkazi wa Kimara kwa tuhuma za mauaji ya mtu aliyedaiwa kuwa mpenzi wake ambaye alikuwa ni kondakta.


Akizungumza Agosti 17, 2022, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Jumanne Muliro, amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya kutoroka na kukimbilia mkoani Lindi akidaiwa kumuua mpenzi wake aliyetambulika kwa jina la Sharifa ambaye alikuwa ni kondakta.


Aidha Muliro ameeleza kuwa katika hatua nyingine wamemkamata Gama Swai, anayetuhumiwa kwa kuuza spea za magari zinazodhaniwa kuwa vifaa vilivyoibwa kwenye magari ya wananchi.

Via >EATV
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top