HAMUTAKIWI KUJIFICHA HATA NYINYI MUNA HAKI YA KUHESABIWA LICHA YA ULEMAVU MULIONAO- WAZIRI BI. HARUSI.

Hassan Msellem
0

Watu wenye ulemavu kisiwani Pemba wametakiwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la kuhesabu watu na makaazi ‘Sensa’ linalotajiwa kuanza Agosti 23 ili nao waweze kujumuishwa katika mipango ya maendeleo.



Mapema akizungumza na viongozi wa jumuiya mbali mbali za watu wenye ulemavu huko katika ukumbi wa idara ya mazingira Machomanne kisiwani Pemba, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman, amesema Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza na kuwapa kipaumbele watu wenye ulemavu nchini ili waweze kujumuishwa katika mipango ya maendeleo ya Serikali.


Aidha, amewaomba wazazi na walezi kutokuwaficha watoto wenye ulemavu pamoja na kuficha aina ya ulemavu walionao ili waweze kupatiwa haki yao ya msingi ya kuhesabiwa.


“Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi kasisitiza sana na katupa kipaumbele cha kutosha kwamba jamai muhakikishe munawafikia watu wenye ulemavu kwani ni watu muhimu katika mipango ya maendeleo na akasema sote ni walemavu watarajiwa” alisema


Sambamba na hayo, amewaomba viongozi hao kupambana na vitendo vya udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu ili kuhakikisha wanaepukana na janga la udhalilishaji ambalo linaonekana kukithiri visiwani Zanzibar.


“Lakini niwaombe tuwe tayari kupambana na hili janga la udhalilishaji ambalo limeingia katika nchi yetu, wanadhalilshwa watu wenye nguvu zao, wenye macho yao, wenye viungo vyao, wenye akili zao seuze sisi ambao tuna mapungufu fulani, kwahivyo niwaombe ndugu zangu tulisimamie kwa pamoja” alisema


Kwa upande wake, mwenyekiti wa watu wasio ona Zanzibar kisiwani Pemba Suleiman Mansour, amesema watu wenye ulemavu kisiwani Pemba wamelipokea vyema zoezi Sensa na kuomba makarani wa Sensa kuwa kauli nzuri kwa watu wenye ulemavu ili kufanikisha zoezi hilo ipaswavyo.


Pia, amemuomba Mheshimiwa waziri kufikisha salamu na ombi kwa Mheshimiwa rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuwaangalia kwa jicho la huruma watu wenye ulemavu ikiwemo kuwajengea ofisi zenye kuendana na mahitaji yao.


Yahya Mohammed Seif ni mtu mwenye ulemavu wa uziwi, ameiomba Ofisi ya mtakwimu mkuu wa kutoa takwimu za watu wenye ulemavu ili waweze kutambua idadi ya watu wenye ulemavu nchini na aina ya ulemavu walionao.


Nae, katibu wa jumuiya ya wasioona Wilaya ya Chake Chake Said Abdalla Sadi, ameahidi huwashajihisha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa pamoja kupambana hali na mali dhidi ya vitendo vya udhalilishaji kwa watu wenye uelamavu.

Mratibu wa Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu Kisiwani Pemba Mashavu Juma Mabrouk, akiwasihi washiriki wa Mkutano huo kutoa mashirikiano Kwa makarani wa sensa.


Zoezi la Sensa ya watu, makaazi linatarajiwa kuanza Agosti 23 kuanzia saa za usiku.


Sense kwa maendeleo, jiandae kuhesabiwa.


Mwisho.

 

-

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top