ITUMIENI VYEMA FURSA YA LUGHA KATIKA SOKO LA UTALII MUTAFANIKIWA- DC MJAJA

Hassan Msellem
0

Wahitimu 16 wa darasa la lugha na utalii wameombwa kiutumia vyema fursa ya lugha za kigeni walizojifunza katika soko la utalii ili mafunzo hayo yaweze kuwaletea maendeleo.


 

Akihutubia katika mahafali hayo huko katika skuli ya sekondari ya Uweleni Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Mheshimiwa Khatib Juma Mjaja, amesema lugha ndio fursa pekee ambayo inatoa fursa nyingi za ajira katika soko la ajira, hivyo basi amesema kuanzishwa kwa kituo hivyo vya lugha za kigeni kutasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza soko la utalii nchini.

 

“Ni waombe sana kuitumia fursa hii lugha katika kujiajiri katika sekta ya utalii ambayo ina fursa za kutosha kwa vijana ambao wana uwezo nzuri wa kuzungumza lugha zaidi ya moja lakini kujiajiri kwenu kutaleta ushawishi kwa vijana wengine kupata moyo wa kujiunga na darasa hili” DC Mjaja


Baadhi ya wanafunzi waliyohitimu Mafunzo ya Lugha na Utalii.


Kwa upande wake, mwenyekiti wa mahafali hayo, Abdalla Saleh Issa, amesema lengo la kuanzishwa darasa hilo ni kuwawezesha vijana katika umahiri wa kuweza kutumia lugha mbali mbali za kigeni ili kuendana na soko la utalii ndani na nje ya Zanzibar.

 

Ameongeza kuwa, wazo la kuanzishwa kwa darasa hilo la lugha limetokana na Mkuu wa Wilaya ya Mkaoni Mheshimiwa Khatib Juma Mjaja wakati alipokuwa afisa mdhamini wizara ya Utalii na Mambo ya Kale kisiwani Pemba, ambapo wazo hilo limefanikiwa kuwasaidia vijana zaidi ya 50 kutoka wilaya ya Mkoani.

 

“Lakini ndugu wahitimu munaemuona hapa licha ya kuwa mgeni rasmi alikuwa ndio afisa mdhamini wizara ya utalii na mambo ya kale, kwahivyo madarasa haya yaliasisiwa chini yake ilikuwa ni rai yake yaanzishwe madarasa haya” Alisema


Nao, wahitimu wameahidi kufanyia kazi ipaswavyo mafunzo ikiwemo kujiendeleza kimasomo sambamba na kujiajiri katika sekta ya utalii.

 

Mwenyekiti wa mahafali, Abdalla Saleh Issa.


Lugha zinazofundishwa katika darasa hilo ni pamoja na lugha ya Kiarabu, Kiingereza, Kifaransa pamoja na Kitaliano.

 

Hayo ni mahafali ya tatu (3) tangu kuanzishwa kwa kituo hicho cha lugha za kigeni na utalii Mtambile.



Jumla ya wanafunzi 16 wamehitimu darasa la lugha za kigeni na utalii na kutunukiwa vyeti vitakavyo wawezesha kujiendeleza na masomo ya lugha mbali mbali pamoja na kuomba ajira katika soko la utalii.

Baadhi ya wazazi wa wanafunzi walioshiriki katika mahafali hayo.


Mwisho.

 

 

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top