MADIWANI WATANO MTWARA WATUMIWA BARUA ZENYE JUMBE ZA VITISHO ZILIZOANDIKWA KWA MAANDISHI MEKUNDU.

Hassan Msellem
0

Madiwani watano Manispaa ya Mtwara Mikindani, Mkoa wa Mtwara wamepigwa na butwaa baada ya kukuta barua zenye ujumbe zilizoandikwa kwa maandishi mekundu nyumbani kwao.



Jumbe zilizosomeka “Munatualibia maisha yetu na nyinyi mujiandae kuhalibiwa kwa namna yoyote maisha yeny” jumbe hizo zimendikwa kwa wino mwekundu huku mwishoni zikiwa na jina la diwani aliyekusudiwa.

 

Jumbe hizo zimebandikwa katika nyumba zao  juzi usiku Agosti 2, 2022.

 

Akizungumzia ujumbe hiyo, Maya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Shadida Ndile, alisema ameshangazwa na ujumbe huo ambao mwishoni umeandikwa jina lake.

 

Amesema kila mmoja alikuta ujumbe ukiwa kwenye bahasha umewekwa nyumbani kwake huku akisema jumbe hizo hazina lengo zuri kwao kwa kuwa umelenga kuwatisha kwa jambo ambalo hawalijui.

 

“Sijui wanamaanisha nini ni ujumbe huo yaani umekuwa wa vitisho kwangu sijui waliondika wanamaanisha nini na kwanini walenge madiwani watano nikiwemo mimi” alisema

 

Alliendelea kusema “Niliupata nilishtuka sana nilipowasiliana na baadhi ya madiwani nao wakawa na ujumbe ule tulifika polisi kutoa taarifa ambao ni madiwani wa kata za Mtonya, Vigaeni, Chuno, Naliendele na Ufukoni”

 

“Unajua Mtwara hatujafikia hatua hiyo tuko salama na shughuli za maendeleo zinaendelea, sio utamaduni wetu kutishana kama kuna watu ambao wamekwazwa na jambo watoe taarifa kwenye mamlaka husika jambo hilo litafutiwe ufumbuzi sio sawa kutishiana na unaemtishia hajui nini kosa lake” Shadida Ndile Meya Manispaa ya Mtwara Mikindani

 

Naye Diwani wa Vigaeni, Said Nassoro alisema jambo hilo ni kubwa.

 

“Mimi sielewi kwanini wamefanya hivyo kwa upande wangu sielewi kwanini mtu aseme kuwa tumemuharibia maisha na sisi tujiandae kuharibiwa maisha yetu ni ujumbe mfupi lakini ni ujumbe ambao unazua maswali mengi kwangu” alieleza

 

“Huu ujumbe aliona mwanangu akanipigia simu kuna ujumbe na akapiga picha akanitumia nikashangaa kwanini barua zinafanana na ndani ya bahasha kulikuwa na barua mbili yangu na Meya hii ni kutishia amani ya mtu kama mtu kaweza kuja nyumbani kwako na kuweka ujumbe huo anaweza kuja kufanya lolote” Said Nassoro

 

Mwananchi ilifanya jitihada za kumpata kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Nichodemus Katembo ambaye alisema hana taarifa za barua hizo na atalifanyia kazi suala hilo.

 

Habari na Mwananchi.

 

Mwisho.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top