MAMA ANUSURIKA KUUAWA NA MUME WAKE ALIYEACHANA NAE MIAKA 17 ILIYOPITA

0

Mariamu Ramadhani na watoto wake 5 wakazi wa wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, wamenusurika kuuawa na mtalaka wake walioachana miaka 17 iliyopita


Inaelezwa kuwa mwanaume huyo alifika nyumbani kwa mwanamke huyo akiwa na Panga, Kisu na Sururu ambapo mwanamke aliamua kukimbia kabla ya mwanaume huyo kuanza kubomoa nyumba na kuiba baadhi ya mali.


Baadhi ya mashuhuda wameliomba Jeshi la Polisi Kiteto kufuatilia tukio hilo ili liwe fundisho pamoja na kwamba vitendo vya ukatili Kiteto vimetajwa kukithiri.

Hata hivyo baada ya mtalaka huyo kutoweka katika mazingira hayo mwanaume huyo aliishia kubomoa nyumba kisha kuingia ndani na kuchukua fedha taslimu shilingi laki mbili za mtalaka na kutoweka kusikojulikana
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top