UKATILI: MLEMAVU MCHUUZI AUAWA KIKATILI MBELE YA UMATI.

Hassan Msellem
0

Mchuuzi wa biashara ndogo ndogo mtaani mwenye ulemavu wa viungo raia wa Nigeria, Alika Ogorchukwu 39, amepigwa hadi kufa huku mashuhuda wakirekodi tukio hilo lililotokea kwenye barabara kuu ya maduka nchini Italia, bila kutoa msaada wowote.


Muitaliano wa Fillipo Ferlazzo 32, alimkaba koo raia huyo wa Nigeria na kumsababishia kifo kwa kukosa hewa.

 

Mauwaji ya Ogorchukwu, yamewashitua watu wengi wakiwemo raia wa nchi hiyo ya Italia, huku video za tukio hilo zikisambaa kwa kasi mitandaoni na kuchapishwa katika tahariri za magazeti, zilizozungumzia tukio hilo kwa kulihusisha na ubaguzi wa rangi.

 

Mbali na raia, wanasiasa wengi wameoneshwa kuumizwa na tukio hilo ingawa kumeibuka kwa wasi wasi kuwa mauaji hayo yanaweza kutumika kama kichocheo cha ubaguzi kabla ya uchaguzi wa kitaifa nchini Italy September 2022.

                                                              

Ogorchukwi, alikumbwa na mkasa huo baada ya kupeleka bidhaa zake kwa Muitaliano Fillipo Ferzallo na kisha kuondoka na baadaye Ferlazzo alimfuata kisha kuchukua fimbo yake ya kutembelea na kumpiga hadi kufa.



Shambulio linadaiwa kutokea eneo la Civitanova Marche, mji wa pwani ya Adriatic, ambapo Februari 2018, mtetezi wa mrengo wa kulia alipiga risasi na kuwajeruhi wahamiaji sita wa Kiafrika katiks eneo la karibu la Macerata.

 

Miaka miwili kabla ya hapo, mwanamme mmoja wa Nigeria pia aliuawa katika eneo la Fermo, ambako lipo upande wa kusini, baada ya kujaribu kumtetea mke wake dhidi ya matusi ya kibaguzi.


Mama wa Alika Agorchukwa akipewa pole na raia wa Italia. 


Mama mzazi wa Alika Ogorchukwi, alilia kwa uchungu huku baadhi ya raia wa Italia wakimpa pole kwa kifo cha mwanae katika eneo 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top