MWALIMU SKULI YA MSINGI MADUNGU PEMBA ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MWANAFUNZI.

Hassan Msellem
0

Mwalimu wa skuli ya msingi Madungu Chake Chake Pemba, alinayefahamika kwa jina la Ali Makame Hatib mwenye umri wa miaka 25, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasla la tano mwenye umri wa miaka kumi na moja (11) jina limehifadhiwa.

Picha kutoka Maktaba.

Akisimua chanzo kilimuwezesha kugundua kwa mtoto wake kufanyiwa kitendo cha udhalilishaji, mama wa mwanafunzi huyo alisema, siku ya Jummane ya tarehe 16, 2022  wakati mtoto wake akisikiliza kipindi cha Kul-haku cha Radio Annour fm mtoto wake alisikia mada kuhusu udhalilishaji, ndipo mtoto huyo aliporuka na kumuambia mama yake kuwa ameshadhalilisha na mwalimu Ali Makam Hatib kwa siku kadhaa kutokana na vitendo alivyokuwa anamfanyia

 

“Ilikuwa siku ya Jumanne ya tarehe 16, 2022 mwanangu akiwa anasikiliza kipindi cha Kul-haku kinachorushwa na Radio Annour kulikuwa na mada kuhusu udhalilishaji akawa anasikiliza vile watangazaji wanavyo zungumza kuhusu mada hiyo kisha kuruhusu watu kupiga simu na kuchangia ndipo, mwanangu aliporuka na kuniambia mama kama ni hivyo mimi nimeshadhalilisha, ni kamuuliza haya kundhalilishwa nani? Akinambia nimedhalilishwa na teacher Ali, basi pale pale nikamuuliza haya teacher Ali kankudhalilisha vipi? Akaniambia akaniambia hivi, kama teacher Ali alikuwa katika kunipiga alikuwa akinikunja nguo na kunichezea sehemu zangu za siri napia alikuwa akinivua nguo sehemu ambazo wanafunzo wangu hapo, baada ya hapo nikamchukua hatua ya kwenda Kituo cha Polisi nilipofika polisi wakaniambia mkono kwa mkono nikaenda mkono kwa mkono na kufanyia mahojiano na kisha kuchunguzwa na kuonekana ameshaharibiwa” alisema mama mwanafunzi huyo

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa kusini Pemba kamishna msaidi za Polisi Abdalla Hussein Mussa, amethibitisha kumtia mbaroni mwalimu huyo na kuahidi kufikishwa mahakamani pindi upalelezi utakapo kamilika.

 

“Ni kweli tunamshikilia mwalimu wa skuli ya msingi ya Madungu anayefahamika kwa jina la Ali Makame Hatib mwenye umri wa miaka 25 akithumiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka kumi na moja, tukio hilo limetokea mnamo tarehe 12 mwezi wa 08 mwaka 2022 majira ya saa 11:30 za jioni huko maeneo ya skuli ya Mdungu ambapo alimuingilia kimwili mwanafunzi huyo na atafikishwa mahakamani uchunguzi utakapokamilika, wito wangu kwa wananchi kwamba tutii sheria bila ya shuruti na vile vile tuwaache hawa wanafunzi wasome  ili baadae wawe ndoto nzuri maishani mwao” alisema

 

Inasemekana hili ni tukio la tatu la ukabaji kufanywa na mtuhumiwa huyo.

Hadi idawaonline.com inatuma taarifa hii mtuhumiwa anashikiliwa katika kituo cha Polisi Madungu na atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.


kubakwa kwa mwanafunzi huyo wa darasa la tano (5) kuna timiza idadi ya wanafunzi nane (8) wa skuli ya msingi kubakwa kisiwani tangu kuanza kwa mwaka 2022 kwa mujibu wa ripoti ya wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar.


Mwisho.

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top