BABA WA MIAKA 50 AHUKUMIWA KWENDA CHUO CHA MAFUNZO (JELA) MIAKA 20 KWA KOSA LA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA SABA.

Hassan Msellem
0

BABA WA MIAKA 50 AHUKUMIWA KWENDA CHUO CHA MAFUNZO (JELA) MIAKA 20 KWA KOSA LA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA SABA.



Mahakama maalumu ya makosa ya udhailishaji Chake Chake, imemuhukumu kutumikia chuo cha mafunzo (Jela) kwa muda wa miaka ishirini (20), Suleiman Rashid Juma almaarufu kwa jina King anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 50, mkaazi wa Pujini kwa kosa la kumlawiti mvulana wa miaka saba.


Hukumu hiyo, imetolewa juzi tarehe 22\08\2022 na hakimu wa mahakama maalumu ya makosa ya udhalilishaji Muumini Ali Juma.


Awali ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka wa Serikali Ali Amour Makame, kuwa siku tarehe 25\03\2022 majira ya saa 5 za asubuhi huko Pujini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, mtuhumiwa alimlawiti mtoto wa kiume wa miaka saba Jambo ambalo ni kosa kisheria kwa sheria nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar kifungu cha sheria nambari 115(1).


Idadi ya mashahidi sita (6) ikiwemo mtoto mwenyewe ambaye ni muathirika wa kitendo hicho, mwanafunzi wa darasa la kwanza anayesoma darasa moja na muathirika, Baba Mzazi wa muathirika, Askari mpelelezi, Daktari dhamana wa hospitali ya Chake Chake na Mkaguzi msaidizi wa jeshi la Polisi shehia ya Pujini Kunvini, ushahidi ambao ulitosha kumtia hatiani mshitakiwa.


Akisoma hokum hiyo, hakimu wa mahakama ya makosa ya udhalilishaji Chake Chake Muumini Ali Juma, amesema kwavile mshitakiwa hilo ni kosa lake la kwanza pamoja na kuzingatia ombi la mshitakiwa kutokana na umri wake na hali yake, hivyo mahakama hiyo imezingatia kifungu cha 299 cha sheria katika utoaji wa adhabu wa kosa hilo pamoja na kifungu cha 314 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sheria ya Zanzibar, sheria nambari saba (7) ya mwaka 2018 kwa mujibu wa kifungu cha 115 (1) sheria nambari sita (60 ya mwaka 2018 Sheria ya adhabu ya makosa  ya jinai, ambapo kosa hilo adhabu ya kifungo cha maisha lakini kwa kuzingatia ombi la mshitakiwa amepewa adhabu ya kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka ishirini pamoja na kulipa fidia ya shilingi milioni moja kwa muathirika.


Ikumbukwe kuwa, tarehe 29\03\2022 kipindi cha Mawio kiliripoti juu ya mshitakiwa huyo kushikiliwa katika kituo cha polisi Madungu kutokana na tuhuma za kumlawiti mvulana huyo, ambapo kwa mara ya kwanza mshitakiwa huyo alifikishwa mahakamani na mnamo tarehe 06\04\2022 dhidi ya shitaka hilo.


Haki ya rufaa imetolewa kwa upande usioridhishwa na hukumu hiyo.

Mwisho.

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top