NYUKI WAVAMIA SHULE, WAJERUHI WALIMU NA WANAFUNZI

0

 

Picha haihusiani na habari hapa chini

KUNDI la nyuki ambalo halikujulikana limetokea wapi limezua taharuki baada ya kuvamia Shule ya Msingi ya Kamena Wilaya ya Liwale mkoani Lindi na kujeruhi walimu na wanafunzi.

Taarifa kutoka wilayani humo na kuthibitishwa na mmoja wa walimu wa shule hiyo, Rehema Mwaitenda, zinaeleza tukio hilo lilitokea saa nane mchana, Julai 26, mwaka huu.

Mwaitenda alisema siku ya tukio, yeye na walimu wenzake wakiwa wanaendelea na majukumu yao ya kikazi, kundi hilo la nyuki lilivamia shuleni hapo na kuwashambulia walimu na wanafunzi.


Alisema katika uvamizi huo, wanafunzi wanane pamoja na walimu wawili walikimbizwa Hospitali ya Wilaya mjini Liwale na kupatiwa matibabu baada ya kung’atwa na nyuki hao.

Chanzo - Nipashe
TAZAMA VIDEO HII YA NAMNA YA KUJITENGENEZEA PESA

MTANDAONI

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top