Mwanafunzi wa darasa la sita, Marko Sanga (12) Mkazi wa Kijiji cha Maleutsi Wilaya ya Makete Mkoani Njombe amekutwa amejinyonga kwa madai kuwa ni kutokana na redio, nguo za shule pamoja na madaftari yake kuungua kwa shoti ya umeme.
![]() |
RPC NJOMBE-Hamis Issa |
Amesema Marko alifungua ng’ombe kama alivyoagizwa na kisha akaenda kujinyonga “Tuliporudi nyumbani tulimtafuta na kumkuta akiwa amefariki huku akining'inia kwenye mnyororo wa baiskeli tunahisi kuungua kwa radio na baadhi ya vitu vyake inaweza kuwa ni sababu ya kujinyonga kwake maana mpaka tunaagana shambani alikuwa katika hali ya kawaida"
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka Wazazi kuishi vizuri na Watoto wao kwani inawezekana Mtoto huyo alikuwa anahofia kuadhibiwa kwa kile kilichotokea ndipo akaona ni heri kufariki