RAIS WA MAREKANI JOE BIDEN ATOA KAULI NZITO KIFO CHA KIONGOZI WA KUNDI LA AL QAEDA.

Hassan Msellem
0

Rais wa Marekani Joe Biden amehutubia taifa la Marekani na kutoa kauli nzito juu ya kifo cha kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda Ayman Al-Zawahiri, aliyeuawa na ndege ya Marekani isiyokuwa na rubani.




Rais Biden, amesema kuwa kifo  cha Al-Zawahiri ni malipo ya unyama alioufanya kwa wananchi wa Marekani kufuatia kuhusika katika utekelezaji wa shambulio la kigaidi la September 11 mwaka 2001 ambalo liliua zaidi ya raia 3000 nchini humo.

 

Aidha kiongozi huyo wa kundi la kigaidi ambaye ana asili ya Misri aliuawa majira ya asubuhi wakati akiwa katika nyumba yake kwenye mji wa Kabul ambapo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Rais Biden ni kwamba hakuna mtu mwengine yetote Yule kutoka katika familia ya Al-Zawahiri ayeathirika au kujeruhiwa katika shambulio hilo.

 

Al-Zawahiri aliuawa vipi?




Maafisa wa Marekani wanasema Zawahiri alikuwa anasimama kwenye veranda ya nyumba yake ya mafichoni. Ghafla, Ndege asiyokuwa na rubani, inayofahamika kama drone- ilidondosha makombora mawili.

 

Taarifa inasema kuwa kombora lilimpiga Zawahiri ambaye alikuwa amesimama nyumbani kwake.

Ndugu wengine wa familia ya Ayman Al-Zawahiri walikuwepo pamoja naye katika eneo hilo, lakini hakuna mtu mwengine aliyeuawa wala kujeruhiwa katika shambulio hilo, na kiongozi wa AL-Qaeda akafa mara moja pale pale peke yake, Maafisa walisema

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top