TAMWA YAKUTANA NA WANA MTANDAO WA KUPINGA VITENDO VYA UDHALILISHAJI PEMBA KUJADILI RIPOTI YA ROBO MWAKA 2022.

Hassan Msellem
0

Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa  Zanzibar, kimesema licha ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuanzisha mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji bado vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia vimekuwa vikiongezeka kwa kasi nchini.



Kauli hiyo imetolewa na mratibu wa Tamwa Kisiwani Pemba Fathiya Mussa Said katika mkutano huo na wana mtandao wa kupinga vitendo vya udhalilishaji Pemba, amesema utafiti wa kihabari uliofanywa Tamwa Zanzibar, mwaka 2020 umebaini kuwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia bado ni tatizo linaloikabili Zanzibar, ambapo jumla ya kesi 788 zimeripotiwa katika Wilaya zote za Unguja na Pemba.


Ameongeza kuwa, miongoni mwa sababu zinazopelekea kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia ni pamoja na matumizi mabaya mitandao ya kijamii, kukaa vijiweni pamoja na utumiaji wa dawa za kulevya.

 

“Ripoti ya Tamwa Zanzibar ya mwaka 2020 imabainisha kuwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia bado ni tatizo sugu, ambapo jumla ya kesi 788 Zanzibar zimeripotiwa kuanzia mwezi January hadi May, hii ikijumisha matukio ya ubakaji 692, kulawiti 100 na kunajisi 96 ambapo wahanga ni watoto walio chini ya umri wa miaka 18” alisema


Akiwasilisha ripoti ya kota ya pili kuanzia mwezi January hadi May, katibu wa wana mtandao kutoka wilaya ya Mkoani Shaaban Juma Kassim, amesema kuanzia mwezi January hadi May 2022, jumla ya kesi kumi (10) zimeripotiwa ambapo miongoni mwa kesi hizo kesi tatu (3) zimeondolewa, kesi mbili (2) ziko katika Polisi, kesi mbili (2) zimesuluhishwa kwenye familia, moja (1) mtuhumiwa ametoka, moja (1) iko kwa mwendesha mashtaka na moja (1) ikisalia mahakamani.

 

“Katika ripoti hii tumefanikiwa kurekodi matukio kumi ambayo yanatoka katika shehia mbali mbali kesi nyingi zilizoripotiwa ni kesi za ubakaji, shambulio la aibu pamoja na utelekezaji” alieleza



Katibu wa Wana Mtandao Wilaya ya Mkoani, Shaaban Juma Kassim, akiwasilisha ripoti ya robo mwaka pamoja na muendelezo wa kesi za ripoti zilizopitwa.

Siti Faki Ali mwana mtandao kutoka Wilaya ya Wete, amesema katika pindi cha mwaka January hadi May 2022, jumla ya kesi 29 ambapo kesi za kubaka kumi na nne (14) kutorosha sita (6) shambulio la aibu nne (4) ujauzito moja (1) kumuingilia maharimu nne (4).


Aidha, amesema kutoka mwezi June hadi Agosti 2022, wamefanikiwa kuripoti kesi kumi na tatu (13) ambapo kesi za kubaka ni saba (7) kutosha moja (1) udhalilishaji wa kingono moja (1) kumpa mimba mwari nne (4).


Wana Mtandao kutoka Wilaya Mkoani na Wete wakifuatilia uwasilishaji wa ripoti ya robo mwaka kutoka Kwa Wana Mtandao wenzao.

Nae, afisa wa dawati la jinsia Wilaya ya Mkoani, amesema miongoni mwa changamoto zilizojitokeza katika kupambana na kesi za udhalilishaji ni pamoja wanajamii kuzisuluhisha kesi hiyo wenyewe na endapo wakishindwa kukubaliana ndipo wanakwenda katika vyombo vya sheria, jambo ambalo linapelekea watuhumiwa kutoroka.


Sambamba na hilo, amesema suala la kukataa kutoa ushahidi kwa waathirika wa vitendo vya udhalilishaji pamoja na mashahidi ni miongoni mwa changamoto zinazozikabili kesi hizo, kwani kukosekana kwa ushahidi kunapelekea kesi hizo kufutwa.


Afisa Habari na Mawasiliano kutoka Tamwa, Pemba Gaspery Charles, akitoa maelekezo ya jinsi ya kupiga na kuandika maelezo ya picha Kwa Wana Mtandao.


Ripoti hiyo ya robo mwaka ambayo pia ilikuwa na muendelezo wa kesi mbali mbali zinazoendelea mahakamani na zile zilizoripotiwa vituo vya Polisi, imetolewa na wana mtandao kutoka wilaya Wete na Wilaya ya Mkoani Pemba, ambapo imeonesha kasi ya vitendo vya udhalilishaji wa kingono na kijinsia kuendelea kushamiri.


Mradi huo wa miaka miwili (2) wa kutumia jukwaa la habari kumaliza udhalilishaji Zanzibar, unatekelezwa na chama cha waandishi wa habari Tanzania ‘Tamwa, Zanzibar, ambao unafadhiliwa na Shirika la kimataifa la maendeleo la Denmark (DANIDA) kupitia ubalozi wa Denmark Nchini.


Mwisho.

 

 

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top