WANAFUNZI 19 WA KIDATO CHA KWANZA WALIOFAULU MICHEPUO 2021, KUTOKA SKULI NNE ZA JIMBO LA CHAMBANI WAZAWADIWA MIKOBA NA VIONGOZI WA JIMBO HILO.

Hassan Msellem
0

WANAFUNZI 19 WA KIDATO CHA KWANZA WALIOFAULU MICHEPUO 2021, KUTOKA SKULI NNE ZA JIMBO LA CHAMBANI WAZAWADIWA MIKOBA NA VIONGOZI WA JIMBO HILO.


Wanafunzi kumi na tisa (19) kutoka skuli nne za jimbo la Chambani waliofaulu darasa la sita mwaka 2021, wameombwa kuzidisha juhudi katika masomo ili kuendelea kufanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne.


Mapema akikabidhi zawadi ya mikoba kwa wanafunzi hao, Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Wilaya ya Mkaoni Ndugu Ali Juma Omar, amesema viongozi wa jimbo hilo wana nia ya dhati ya kuwaisadia sekta ya elimu, hivyo basi amewaomba wanafunzi hao kuzidisha juhudi ili kuendelea kufanya vyema katika masomo yao.


“Ndugu wanafunzi naomba niwahakikishie kuwa viongozi wa jimbo hili ambao ni Mheshimiwa Mbunge, mwakilishi pamoja madiwani wana nia ya dhati na kweli ya kuwasaidia wanafunzi wa jimbo hili hususan wale wanaofanya vizuri, hivyo basi munapaswa kuongeza juhudi ili kuwaunga mkono” alisema


Aidha, amewataka wanafunzi hao kujiepusha na matumizi mabaya ya simu za mkononi na badala yake kuzitumia kwa malengo mazuri ikiwemo kujifunza mambo mbali mbali yanayoendana malengo yao.


“Niwaombe sana juu matumizi ya simu hususan hizi smartphone, simu hizi zina mambo mengi sana mazuri na mabaya ni juu yako kuchagua unataka kuitumiaje, kwa hivyo nawaomba sana kwa wale wwnye simu kubwa kuzitimia vizuri simu hizi katika kujifunza mambo mbali mbali yanayoendana malengo yenu” Ali Juma Nassor


Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkoani Ndg. Ali Juma Nassor, akizungumza na wanafunzi waliofaulu darasa la sita 2021.


Kwa upande wake, Katibu wa jimbo la Chambani Amour Kheri Vuai, amewasihi wanafunzi hao kutokujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi kwani kufanya hivyo kupelekea kutokufanikiwa kimasomo pamoja na kukatisha ndoto zao.


“Niwaahidi kuwa mwanafunzi yeyote ambaye atajiingiza katika mambo ya mapenzi ni vigumu kufanya vizuri katika masomo yake, kwasababu muda mwingi huutumia katika kufikiria mapenzi badala ya masomo, kwa hivyo nawaomba sana kutokujihusisha na mapenzi nyinyi sasa hivi kazi yenu ni moja tu ya kusoma basi” aliwasihi


Nae, mwalimu mkuu wa skuli ya msingi Ngwachani Asha Haroun Abdalla, amewashukuru viongozi wa jimbo la Chambani kwa kujitoa kwao kuisaidia sekta ya elimu katika jimbo na kuwaomba kuendelea na moyo huo ili kukuza sekta ya elimu katika jimbo hilo.


Mwalimu Mkuu wa Skuli ya msingi Ngwachani, Asha Haroun Abdalla, akitoa neno la shukurani kwa Viongozi wa Jimbo la Chambani.

“Niwapongeze sana viongozi wetu wa jimbo la Chambani kwakweli wanajitoa sana katika kuisaidia sekta ya elimu katika jimbi hili, ni waombe waendelee na moyo huu huu ili kuhakikisha sekta ya elimu katika jimbo hili inafanya vizuri” mwalimu mkuu


Nao, wanafunzi hao wameahidi kusoma kwa bidii ili kuhakikisha wanafanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne na sita.


Wanafunzi waliofaulu darasa la sita 2021 kutoka Skuli nne za Jimbo la Chambani.


Skuli hizo nne (4) ambazo zimefanikiwa kufaulisha wanafunzi hao wa darasa la sita (6) mwaka 2021 ni Skuli ya msingi Ngwachani ambayo imefaulisha wanafunzi kumi na nne (14) Skuli ya msingi ukutini wanafunzi wawili (2) Skuli ya msingi Dodo wanafunzi (2) na Skuli ya msingi Mizingani mwanafunzi mmoja (1) na kuifanya idadi ya wanafunzi kuwa kumi na tisa (19).

Mwisho.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top