WAZAZI WATAKIWA KUWADHIBITI WATOTO WAO KUSHIRIKI UCHUMAJI WA ZAO LA KARAFUU.

Hassan Msellem
0

Wazazi Mkoa wa Kusini Pemba wametakiwa kuwadhibiti watoto wao kutokushiriki uchumaji wa zao la karafuu ili waweze kuendelea  na masomo yao  na kuwakinga na vitendo vya  udhalilishaji.


Akizungumza na  na masheha  pamoja na wakulima wa zao la karafuu katika ukumbi wa makonyo  Wawi na ZSTC Mkoani Mkuu wa Mkoa wa Kusinie Pemba Mhe. Matar Zahor Massoud, amesema wakati wa mavuno ya karafuu kuna jitokeza vitendo vingi vya udhalilishaji  wa kijinsia  kwa watoto, hivyo ni vyema kwa jamii  kuweka utaratibu wa kuwahamasisha  watoto kuhudhuria masomo.

 

Akizungumzia sheria  na kanuni  za karafuu  katibu wa shirika la biashara la taifa ZSTC Ali Hilal Vuai, amesema shirika hilo  halina wakala wa ununuzi wa karafuu  na atakaebainika  kufanya biashara hiyo pamoja na kutumia nembo ya shirika la ZSTC hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

 

Wakulima wa zao la karafuu, wachumaji, waokota mpeta (karafuu zinazoanguka chini) pamoja na wafanya biashara visiwani Zanzibar wanajiandaa kufaidika na zao hilo kwa msimu wa mwaka.

Zao la karafuu huchumwa kwa mwaka mara mbili kupitia msimu wa Vuli na mwaka.

Habari na, Zbc radio.

KAMA HUKUTAZAMA VIDEO HII YA MWENYEKITI WA CCM KUTAKA WANAUME WAOE WANAWAKE WENGI BOFYA SASA



Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top