BARAZA LA MADIWANI MAKETE LAWAFUTA KAZI WATUMISHI 4 KWA UBADHILIFU WA FEDHA

0

 Waliokuwa watumishi wanne (4) katika Halmashauri ya Wilaya ya Makete wamefukuzwa kazi kwa ubadhirifu wa fedha za Mapato ya ndani na mmoja ni utoro kazini na kuisababishia hasara Serikali.

Maamuzi hayo ni kufuatia Kikao maalumu cha Baraza la Madiwani lilikutana leo kujadili maadili ya watumishi zaidi ya 60 ambapo kati ya hao watumishi wanne wamefutwa kazi na watumishi watano (5) wameagizwa kukatwa mishahara yao 15% kwa mwaka mmoja, wengine miaka miwili na mmoja miaka mitatu

Watumishi waliofukuzwa kazi ni aliyekuwa Mtendaji Kata ya Mbalatse Omega Aloyce Thobias ambaye amefukuzwa kwa utoro kazini kwa kipindi cha siku 214.

Watumishi wengine ni waliokuwa watendaji wa vijiji ambao ni Bryson Isaack Sanga aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Ludihani, Godwin Jacob Luvanda aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Ikuwo na Tumaini Shem Ngogo aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Kigala

Watendaji hao watatu wamefukuzwa kwa ubadhirifu wa fedha za mapato ya ndani ambapo Tumaini Ngogo amekusanya fedha zaidi ya Milioni 44 na kupeleka Bank.

Akizungumza na waandishi wa Habari baada ya Kikao hicho, Mkueugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Makete William M. Makufwe amesema kufuatia kubainika na makosa watumishi hao wamefutwa kazi kuanzia sasa.

“Niwasihi watumishi wengine tuliopo kazini zama za kutumia fedha za makusanyo zikiwa chini ya makusanyo yao zimeshapitwa na wakati na unakamatwa wakati wowote…ukikusanya kuanzia shilingi laki tano hakikisha fedha hizo zinakuwa salama kwa kupeleka Bank ili waepuke kingia kwenye vishawishi vya wizi wa fedha hizo”.

“Kuhusu huyu Mtumishi ambaye amekuwa mtoro kwa kipindi cha zaidi ya siku 200 naye amefukuzwa kazi kwa kutokuwepo kazini wakati taratibu zote za kumfuta kazi zimefanyika kwa kufuata sheria za utumishi”

Kwa niaba ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri (W), Diwani Kata ya Mfumbi Mhe. Atilyo Ng’ondya amesema watumishi wanapaswa kuwa makini na matumizi ya fedha za Serikali kwa kuwa Serikali ina mkono mrefu na vyombo vingi katika kuwasimamia watumishi wake.

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top