MAMA NA MWANA WATOA USHAHIDI KESI YA KUBAKA INAYOMKABILI MWALIMU WA SKULI YA MSINGI MADUNGU.

Hassan Msellem
0

Kesi ya kumbaka mwanafunzi inayomkabili mwalimu wa Skuli ya Msingi Madungu Ali Makame Hatib 25, imeanzwa kusikilizwa ushahidi kwa mara ya kwanza juzi Septemba 05.09.2022, ambapo shahidi nambari moja ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 11 na mama yake mzazi wametoa ushahidi mbele ya hakimu wa Mahakama ya makosa ya udhalilishaji Muumini Ali Juma.


Ilielezwa Mahakamani hapo na Mwendesha mashtaka wa Serikali Seif Mohammed Khamis, kwamba siku ya tarehe 12/08/2022 majira ya saa 11:30 za jioni huko Skuli ya Msingi Madungu Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, Mshitakiwa ambaye ni Mwalimu wa Skuli ya Msingi Madungu Ali Makame Hatib mwenye umri wa miaka 25, alimbaka mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka kumi na moja jina limehifadhiwa jambo ambalo ni kosa kisheria.

 

Kilichozusha hisia kwa watu wote waliokuwepo Mahakamani hapo ni baada ya mshitakiwa kumwaga matone ya machozi huku akisikika akisema kuwa hana tena maisha kutokana na kukaa rumande kwa muda mrefu ambapo itapelekea kufukuzwa kazi.


Ikumbukwe kuwa, kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilitajwa Mahakamani Agosti 22.2022, ambapo mshitakiwa aliamuriwa kwenda rumande hadi tarehe 05.09.2022 kwa ajili ya kusikilizwa kwa ushahidi.

 

Kesi hiyo imeghairishwa hadi tarehe 14.09.2022 ili kuendelea na ushahidi.

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top