KESI YA TUHUMA ZA UBAKAJI INAYOMBAKIBILI MWALIMU WA SKULI YA MSINGI MADUNGU DAKTARI ATOA USHAHIDI.

Hassan Msellem
0

Kesi ya tuhuma za Ubakaji inayomkabili mwalimu wa Skuli ya msingi Madungu aliefahamikwa jina la Ali Makame Khatib mwenye umri wa miaka 25, mkaazi wa Matuleni Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, juzi 20.09.2022 imeendelea kwa kusikilizwa ushahidi kutoka kwa daktari aliyemfanyia vipimo msichana aliyefanyiwa vitendo vya udhalilishaji na mwalimu huyo mara baada ya msichana huyo kufikishwa hospitali ya Chake Chake kwa ajili ya uchunguzi.

Picha kutoka Maktaba


Akitoa ushahidi mbele ya mahakama hiyo daktari huyo amesema kuwa vipimo vya awali alivyofanyiwa mtoto huyo mara baada ya kuripotiwa kwa tuhuma za kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji vimeonesha kuwa mtoto huyo amefanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

 

“Mheshimiwa vipimo vya awali tulivyomfanyia muathirika mara tu baada ya kufikishwa hospitalini vimeonesha kuwa tayari mtoto huyo ameingiliwa katika sehemu zake za siri za mbele kwa mara kadhaa” alisema daktari huyo

 

Ikumbukwe kuwa, kesi hiyo iliripotiwa mahakamani hapo tarehe 05..2022, ambapo ilielezwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Seif Mohammed Khamis, kuwa Agosti 12, 2022 majira ya saa 11:30 za jioni huko katika skuli ya Msingi Madungu, Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, mshitakiwa alimbaka msichana mwenye umri wa miaka 11 anaesoma darasa la tano ambapo ni kosa kisheria.

 

Kesi hiyo imeghairishwa tarehe 03.2022 itakapoendelea na ushahidi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top