MAMA AMGEUZA KITEGA UCHUMI MTOTO WAKE WA MIAKA 8 KWA KUSINGIZIA KUBAKWA ‘NYARUGUSU’

Hassan Msellem
0
Wananchi wa Nyarugusu Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi, wamechoshwa na tabia ya mama mmoja aliefahamika kwa jina la Fatma Khamis Mohammed kutokana na tabia yake ya kuwasingia wananchi wa eneo hilo kumfanyia vitendo vya udhalilishaji mtoto wake wa kike mwenye umri wa miakaq nane (8) ili kujiingizia kipato kupitia faini ambazo zinatozwa katika vituo vya polisi kwa mwananchi anaemsingizia kumfanyia vitendo vya udhalilishaji mtoto wake.

Wakizungumza na kipindi cha Mawio wananchi wa eneo hilo, wamesema wamechoshwa na tabia ya mama huyo ya kumgeuza kitega uchumi mtoto wake kwa kusingizia kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji na wakaazi wa eneo hilo kitendo ambacho wamedai sio cha kweli na kinawaondoeshe heshima na uaminifu.

“Huyu mama ana tabia mbaya sana kila siku anadai mtoto wake amedhalilishwa sijui amebakwa sisi ndio wenyeji wa mtaa huu kwa muda mrefu na hatujawahi kusikia tabia kama hizo, lakini tangu alipokuja kuhamia yeye anasema mtoto wake anabakwa mtoto wenyewe mmoja kwahivyo tumechoshwa na tabia zake tuomba ahamishwe anatutia aibu na kutuvunjia heshima” alisema mama mmoja miongoni mwa wananchi hao.


Mmiliki wa nyumba ambayo amepanga mama huyo, amesema tayari ameshamrudishia fedha zake ambazo alilipia pango pamoja na kumpa siku tatu kuhama nyumbani kwake lakini amejiongezea siku tano za kuendelea kuishi katika nyumba hiyo, hivyo basi ameomba msaada kutoka mamlaka husika ili kumuhamisha mama huyo.

“Ninavyo zungumza hapa ana siku ya nane hajahama kwahivyo anaonesha ni jinsi gani mtu huyo ni mkorofi majirani wananisubiri mimi tu ni waruhusu ili waweze kumtoa” Alisema mmiliki huyo wa nyumba

Amani Ayoub Makame ni Sheha wa Shehia ya Mwanakwerekwe, amekiri uwepo wa tabia hiyo inayofanywa na mama huyo, nakusema amechukua hatua za kutoa taarifa kwenye kituo cha Polisi Kijito Upele na hatua za kumuhamisha  ameshazifikisha kwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini ili kufanyika kwa zoezi hilo.

 “Anakuwa na matusi kwa wanajamii kibaya zaidi ni kwamba kila siku anasema mtoto wake kabakwa kampeleka huyu polisi kampeleka yule polisi, kitu ambacho tumeshindwa kumuhamisha asubuhi alikuwa na mama yake mzazi na alisema anampeleka sehemu ilituweze kufanya muamala lakini mwisho wa safari mapaka kufikia hivi sasa simu yake inaita bila ya majibu lakini nimo katika jitihada za kuwatafuta ndugu zake” alisema sheha huyo.

Juhudi za mawio za kumtafuta mama huyo ili kutoa maelezo juu ya shutuma hizo ziligonga ukuta kutokana na kukataa kutoa ushirikiano.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top