MKUTANO WA NANE WA BARAZA LA WAWAKILISHI KUANZA LEO, MCHEZO WA MASUMBWI ZANZIBAR KUJADILIWA.

Hassan Msellem
0

 Mkutano wa nane wa baraza la kumi na wawakilishi unatarajiwa kuanza leo katika ukumbi wa baraza hilo Chukwani.



Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari katibu wa baraza hilo Bi. Raya Issa Msellem, amesema miongoni mwa shughuli zitakazofanyika  katika kikao hicho ni kujadili wa mswada wa Sheria ya kufuta Sheria namabri 4 ya mwaka 2007 ya baraza la Wawakilishi kuhusiana na kinga, uwezo wa fursa katika utekelezaji wa kazi na mswada wa Sheria ya kuanzishwa kwa taasisi ya wahasibu, wakaguzi na washauri elekezi wa kodi Zanzibar.

 

Aidha kikao hicho, kitapokea kauli ya Serikali kuhusiana na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali kupatiwa majibu maswali 159 yatakayowasilishwa na wajumbe pamoja na kupokea taarifa ya Serikali kuhusiana mchezo wa ngumi Zanzibar.

 

Hivyo basi, Bi. Raya amewaomba wananchi kufatilia kwa karibu yatakayoendelea katika mkutano huo ili kutambua mambo mbali mbali yenye maslahi ya nchi.

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top