MKUTANO WA NANE WA BARAZA LA WAWAKILISHI KUANZA LEO, MCHEZO WA MASUMBWI ZANZIBAR KUJADILIWA.

Hassan Msellem
0

 Mkutano wa nane wa baraza la kumi na wawakilishi unatarajiwa kuanza leo katika ukumbi wa baraza hilo Chukwani.



Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari katibu wa baraza hilo Bi. Raya Issa Msellem, amesema miongoni mwa shughuli zitakazofanyika  katika kikao hicho ni kujadili wa mswada wa Sheria ya kufuta Sheria namabri 4 ya mwaka 2007 ya baraza la Wawakilishi kuhusiana na kinga, uwezo wa fursa katika utekelezaji wa kazi na mswada wa Sheria ya kuanzishwa kwa taasisi ya wahasibu, wakaguzi na washauri elekezi wa kodi Zanzibar.

 

Aidha kikao hicho, kitapokea kauli ya Serikali kuhusiana na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali kupatiwa majibu maswali 159 yatakayowasilishwa na wajumbe pamoja na kupokea taarifa ya Serikali kuhusiana mchezo wa ngumi Zanzibar.

 

Hivyo basi, Bi. Raya amewaomba wananchi kufatilia kwa karibu yatakayoendelea katika mkutano huo ili kutambua mambo mbali mbali yenye maslahi ya nchi.

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top