MWANAFUNZI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI BAADA YA KUKATAA KUOLEWA.

Hassan Msellem
0

Mwanamke mmoja nchini Misri anayefahamika kwa jina Amani Abdul-Karim Al-Gazzar mwenye umri wa miaka 19, ambaye ni mwanafunzi wa elimu ya viungo ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya kukataa ombi la kuolewa na mwanamme aliyemzidi umri.

 


Mwanafunzi huyo alipigwa risasi mgongoni nje ya nyumba yao baada tu ya yeye familia yake kukataa pendekezo la ndoa kutoka kwa Ahmed Abou Ameirah mwenye umri wa miaka 29, ambaye pia alijipiga risasi muda mchache baada shambulio hilo siku ya Jumamosi Septemba 03, 2022.

 

Taarifa kutoka jeshi la Polisi zimeeleza kuwa Ahmed alimuua Amani kwa hasira baada ya yeye na familia yake kukataa pendekezo lake la ndoa kabla ya kukimbia eneo la tukio katika kijiji cha Takh Tanbisha karibu na Mji Mkuu wa Misri, Cairo.

 

Kabla ya kujitoa uhai, mwanamme huyo aliwahi kurekodi video fupi akisema amekuwa akiishi kwa ajili ya mwanamke huyo, hivyo kukataliwa kwake kumemfanya ajisikie vibaya na hivyo lazima atalipiza kisasi.

 

Mauaji hayo ya kutisha yanakuja wakati Misri ikikabiliana na viwango vya uhalifu wa kikatili vinavyoongezeka unaowalenga wanawake, huku kukiwa na kesi nyingi za juu zinazohusisha wanawake ambao walikataa kushawishiwa na wanaume.

Tukio hilo la mauaji linafuatiwa na mauaji ya Naira Ashraf ambaye aliuawa nje ya chuo kikuu cha Kaskazini mwa Misri alipokuwa akielekea kwenye mitihani yake ya mwisho baada ya kukataa mapendekezo kadhaa ya ndoa kwa muuaji wake.

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top