MWANAMKE MWINGINE AUAWA NA WASIOJULIKANA KWA USHIRIKINA

0
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP Janeth Magomi

 

JESHI la Polisi mkoani Shinyanga, linawasaka watu ambao bado hawajafahamika kwa tuhuma za mauaji ya Bibi Sophia Dotto (66) mkazi wa kijiji cha Kazuni Kata ya Bukene wilayani Shinyanga.


Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 2 usiku nyumbani kwa Bibi huyo ambapo watu wasiojulikana, walifika nyumbani kwake na kisha kutekeleza mauaji hayo ya kinyama kwa kumpiga kichwani na vitu vizito na kusababisha mauaji.


Akielezea tukio hilo Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kazuni Juma Shija, amesema Bibi huyo mwenye umri wa miaka (66) alikuwa akiishi yeye na mchungaji wake wa mifugo nyumbani kwake, na ilipofika majira hayo ya saa 2 usiku ndipo yalipotokea hayo akituhumiwa kuwa ni mshirikina.


 “Baada ya kukuta Bibi huyo akiwa amefariki dunia, nilitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ambao walifika kijiji majira ya saa 8 usiku wakauchukua mwili wa marehemu,”amesema Shija.


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kubainisha kuwa upelelezi wa awali inasemekana Bibi huyo ameuawa kwa imani za kishirikina, na kubainisha kuwa Jeshi hilo linawasaka watu wote ambao wamehusika na mauaji hayo.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top