PEGAO YAPOKEA RIPOTI YA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI WANAWAKE KUTOKUSHIRIKI KATIKA NAFASI ZA UONGOZI KUTOKA KWA WAHAMASISHAJI JAMII.

Hassan Msellem
0

Jumuiya ya Mazingira na Utetezi wa Kijinsia Kisiwani Pemba ‘PEGAO’ imepokea ripoti ya miezi mitatu kutoka mwezi April hadi June kutoka kwa wahamasishaji jamii kuhusu mradi wa kuwahamasisha wanawake kugombea nafasi mbali mbali za uongozi pamoja uimarishaji wa demokrasia nchini.



Akipokea ripoti hiyo, Mkurugenzi kutoka jumuiya ya Mazingira na Utetezi wa Kijinsia Pemba ‘PEGAO’ Hafidh Abdi, amewaomba wahamasishaji jamii hao kuongeza juhudi katika kuwafikia wananchi pamoja na kufahamu lengo mahsusi la mradi huo ili liweze kufikiwa ipaswavyo.


“Kwanza munatakiwa muwe na juhudi binafsi katika jambo hili ili kuwafikia wananchi wengi ziadi hususan akina mama ambao ndio tunawalenga zaidi lakini kufahamu lengo letu ni lipi haswa ili tunapokutana na wananchi licha ya kusikiliza changamoto zao tuweze kufanikisha lengo la mradi huu ambalo ni kuwahamasisha akina mama kugombea nafasi mbali mbali za uongozi pamoja na uimarishaji wa demokrasia katika vyama vya Siasa” alisema


Akiwasilisha ripoti hiyo ya mwezi April hadi June, muhamasishaji jamii kutoka Wilaya ya Wete Raya Said Ali, amesema katika Shehia ya Mjananza wananchi wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo akina kutokujua kusoma na kuandika, ukosefu wa Kituo cha Afya, ukoseu wa maji safi na salama, utoro kwa wanafunzi na kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa pamoja na vyeti vya vifo.

 

Ameongoza kuwa, licha ya changamoto hizo asilimia 90 ya akina mama wamekubali kugombea katika nafasi mbali mbali za uongozi na kuomba kupatiwa elimu ili wawe na uwezo wa kugombania nafasi hizo ipaswavyo.

 

“Kwakweli wana shehia ya Mjananza licha ya changamoto zote walizonazo ikiwemo changamoto ya kutokujua kusoma na kuandika lakini wote wamekubali kugombania nafasi mbali mbali za uongozi” Raya Said Ali

 

Siti Habib Mohammed ni Muhamasihaji jamii Wilaya ya Mkoani, akiwasilisha ripoti hiyo, amesema katika Shule ya Kunguni Wambaa inakabiliwa na uhaba wa walimu jambo ambalo linapelekea wanafunzi kutokufika Shuleni kwa wakati sambamba na kutoroka pamoja na kukosa masoma ya uhakika kwa wanafunzi ambao wanasilia shuleni hapo.

 

“Skuli ina marada 13 kuanzia maandalizi hadi darasa la saba, ambapo skuli mzima ina walimu wanawake watatu na walimu wakiume wawili huku wanafunzi 682 ambapo kila mwalimu analazimika kufundisha wastani wa wanafunzi 136 katika mazingira hayo elimu bora itapatikana vipi” alihoji

 

Katika hali isiyo ya kawaida muhamasishaji jamii huyo, amesema katika changamoto nyengine walioibua ni uwepo wa familia ambayo ina watoto watano wenye ulemavu wa viungo katika Kijiji cha Kwa-Azani, ambapo Mama wa familia hiyo amesema anatamani kugombea nafasi mbali mbali za uongozi lakini kutokana na changamoto ya ulezi wa watoto wake wenye ulemavu ndio chanzo cha yeye kushindwa kugombea nafasi za uongozi katika jamii vyama vya siasa.

 

“Kwahivyo katika harakati zetu za kuendelea kuihamasisha jamii tulikutana na huyo mama mwenye watoto watano ambao wote wana ulemavu wa viungo, tulipomtaka agombee nafasi mbali mbali za uongozi amesema hawezi kugombea nafasi za uongozi kutokana na hali ya watoto wake kuwa walemavu na kushindwa kupatiwa msaada wowote kutoka Serikalini wala taasisi binafsi kibaya zaidi imewabidi kukatisha masomo” alisema

 

Amesema, Changamoto nyengine zinazowakabili wananchi wa shehia hiyo ni ubovu wa barabara kutoka Kijiji cha Wambaa hadi Kijiji cha Kutukuu changamoto ambayo inapelekea wananchi wa maeneo hayo kushindwa kufanya shughuli zao za maendeleo ipaswavyo.

Muhamasishaji jamii kutoka Wilaya ya Mkoani Siti Habib Mohammed, akiwasilisha ripoti kuhusu changamoto zinazowakabili wananchi wa Shehia ya Wambaa.


Nae, muhamasishaji jamii kutoka Wilaya ya Michewezi Asha Rashid Abdalla, amesema wananchi wa Shehia ya Kinowe wanakabiliwa na Changamoto ya miundo mbinu bora ya barabara hususah kipindi cha msimu w mvua jambo ambalo linapelekea kudumaa kwa shughuli zinazowaingizia wananchi kipato.

 

Aidha, amesema miongoni mwa changamoto zinazowakabili wananchi hao ni ukosefu wa huduma ya nishati ya umeme pamoja na utoro wa wanafunzi mashule hali inayopelekea kuongezeka kwa vitendo viovu mitaani ikiwemo utumiaji wa dawa za kulevya, wizi na vitendo vya udhalilishaji.

 

Aidha, amesema changamoto nyengine zinazowakabili wananchi hao ni uwepo wav yeti feki vya kuzaliwa, uchache wa fursa za ajira, hali ngumu ya maisha pamoja uchache wa madara na waalimu katika skuli ya Msingi ya Chimba idadi ya madarasa 17, wanafunzi 1024 na walimu 17.

Muhamasishaji jamii kutoka Wilaya ya Michewezi Asha Rashid Abdalla, akiwasilisha ripoti kuhusu changamoto zinazowakabili wananchi wa Shehia ya Kinowe na Chimba, zinazopelekea Akina mama kushindwa kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika vyama vya siasa.


Hasina Omar Salim, ni muhamasihaji jamii kutoka Wilaya ya    Chake Chake, amesema changamoto inayowakabili wa Shehia ya Wara ni maelewano madogo baina ya wananchi wa Kijiji cha Mbuni na Mamlaka ya Maji Zanzibar ‘ZAWA’ changamoto ambayo ametokana na wanakijiji kuona kuwa sio haki kulipia bili ya maji kwa mamlaka hiyo, kwani huduma hiyo wamepatiwa na mfadhili ambaye ni tofauti na mamlaka hiyo.


Akitaja changamoto nyengine, amesema kuporomoka kwa maadili, utumiaji wa dawa za kulevya, unyanyasaji wa kijinsia pamoja na wizi ambao unahusisha vijiji vya Makondeko, Kiumbe Mzito na Ujinga hali ambayo inasababishwa na kukosekana kwa mashirikiano kati ya wanajamii na vyombo vya usalama.


Amesema Changamoto nyengine zinazowakabili wananchi hao ni ubovu wa miundombinu ya barabara za ndani hususan katika Kijiji cha Shimoni, hali inayopelekea changamoto kwa wafanyabiashara kutokufika sokoni bidhaa zao kwa wakati.

Hasina Omar Salim, ni muhamasihaji jamii kutoka Wilaya ya Chake Chake, akiwasilisha ripoti kuhusu changamoto zinazowakabili wananchi wa Shehia ya Tibirinzi na Wara ikiwemo kuporomoka kwa maadili, utumiaji wa dawa za kulevya pamoja na unyanyasaji wa kijinsia.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi huo kutoka ‘PEGAO’ Dina Juma Makota, amewasihi wahawasishaji jamii hao kufuata sheria na kanuni katika utekelezaji wa majukumu yao ili kuepuakana usumbufu unaoweza kutokeza sambamba na kuzingatia malengo ya mradi huo ambayo ni kuwahamasisha akina mama katika kugomania nafasi mbali mbali za uongozi pamoja uimarishaji wa demokrasia katika vyama vya siasa.

 Baadhi ya wahamasishaji Jamii na wadau wa mradi wa kuwawezesha wanawake kushiriki katika Uongozi walioshiriki katika mkutano huo.


Mratibu wa jumuiya ya Kwa ajili ya Watu wenye ulemavu wa akili Pemba Khalfan Amour Mohammed, akiwasihi wahamasishaji Jamii kuzingatia lengo la mradi huo pindi wanapokutana na Wananchi, ambalo ni kuwahamisha Akina mama kujiunga na vyama vya siasa sambamba na kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi na uimarishaji wa demokrasia.


 

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top