RIPOTI YA ‘CAG’ YAMNG’OA KAMISHNA MAKARANI ZAECA.

Hassan Msellem
0

RIPOTI YA ‘CAG’ YAMNG’OA KAMISHNA MAKARANI ZAECA.



Aliyekuwa Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar ‘ZAECA’ Ahmed Khamis Makarani, amejiuzulu baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali ‘CAG’ kuwasilisha ripoti kwa Mhe. Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ripoti iliyoonesha upotevu wa mamilioni ya fedha.


Taarifa ya kujiuzulu kwa Kamishna Makarani, imetolewa na mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Charles Hillary kupitia taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari leo Septemba 02\2022.


“Rais wa Zanzibar amekubali barua ya kujiuzulu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, Ahmed Khamis Makarani”


Imesema taarifa hiyo ikieleza kuwa ni hatua inayofuatia kauli ya Rais Dk. Mwinyi kutaka ZAECA kujitathmini.


Rais DK. Mwinyi aliwataka watendaji wa ZAECA kujitathmini kutokana na ripoti ya CAG kuonesha upotevu mkubwa wa fedha wakati akihutubia hadhara ya viongozi mbali mbali baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Zanzibar ‘CAG’ ya Mwaka 2020/2021.


Dk. Mwinyi akipokea ripoti kutoka Kwa CAG.


Ripoti iyo imeeleza kasoro nyingi za matumizi ya fedha za Serikali zinazosababisha ubadhirfu wa fedha wa mamilioni ya fedha.


Dk. Mwinyi akionesha kukerwa na ufisadi Serikalini alisema anashangazwa kukuta matatizo hayo yanajirudia na hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa kwenye vyombo vya Sheria.


Alisema anashangaa kwamba hakuna kesi hata moja iliyopelekwa mahakamani wakati ofisi yake imekabidhi kwa ZAECA ripoti yenye maelezo thabiti ya namna ufisadi ulivyofanyika na wahusika kutajwa na baadhi yao ukukiri na kurudisha fedha.


“Hatuwezi kuendelea hivi wizi kila mahali na hakuna kesi iliyopelekwa mahakamani kwa namna hii inabidi ZAECA mujitathmini hatuwatendei haki wananchi” alisema Dk. Mwinyi baada ya kusikiliza maelezo ya ripoti ya masaa manne mfululizo kutoka kwa CAG Dk. Othman Abbas Ali akieleza namna mabilioni ya fedha yalivyopotea huku wahusika wakikosa majibu.


Makarani ambaye ni afisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania mwenye cheo cha kamishna msaidizi ‘Assistant Commissioner of Police' (ACP) ambapo kabla ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo alikuwa Kamanda wa Polisi kamishna msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba.


Chanzo. Mwanahalisi.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top